Search This Blog

Friday, September 13, 2013

HATIMAYE LIONEL MESSI AKIRI FRANK RIBERY NDIO MCHEZAJI BORA WA ULAYA KWA SASA

Nyota wa Barcelona  Lionel Messi amekiri kwamba winga wa Bayern Munich Franck Ribery anastahili kushinda tuzo ya mchezaji bora wa ulaya kwa mwaka huu.

Muargentina huyo na Cristiano Ronaldo walikuwa wanashindania tuzo hiyo lakini wakashindwa na Ribery jijini Monaco mwezi uliopita na sasa mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 amesema kwamba mafanikio ya Ribery kushinda makombe matatu yanamaanisha kwamba ndio mchezaji sahihi kutwaa tuzo hiyo.
"Ilikuwa ni heshima kubwa kuwa katika kinyang'anyiro kwa mara nyingine tena, miongoni mwa wachezaji wa tatu bora brani ulaya, aliiambia Uefa.

"Kuna wachezaji wengi wazuri duniani na ni jambo kubwa kushindani lakini kwa hivi ni Ribery anayestahili kushinda tuzo hiyo."

Messi na timu yake ya Barcelona waliondolewa kwenye mashindano ya Champions league msimu uliopita kwa aibu ya kufungwa jumla ya mabao 7-0 na Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment