Search This Blog

Wednesday, June 19, 2013

NIGERIA YABAKI KUWA TIMU PEKEE KUTOFUNGWA KWENYE KOMBE LA MABARA TANGU KUANZISHWA KWAKE BAADA YA KUIPA KIPIGO CHA 6-1 TAHITI

 Timu ya taifa ya Nigeria jana usiku iliitandika TAHITI mabao 6-1 kwenye michuano ya kombe la mabara inayoendelea huko nchini Brazil. Mchezo huo umetengeneza takwimu nyingi sana - zipo kama ifuatavyo:

- Nnamdi Oduamadi ndi mwanasoka wa kwanza wa kiafrika kufunga mabao 3 kwenye mechi moja katika michuano ya Mabara 

 - Jonathan Tehau ndio mchezaji wa kwanza wa Tahiti kwenye michuano ya FIFA 


 - Nigeria wanabaki kuwa ndio timu pekee ambayo haijawahi kupoteza mchezo katika historia michuano hii kwa timu ambazo zimewahi kushiriki. Wakishinda mara mbili na kutoa suluhu mara mbili. 


 - Jonathan Tehau ndio mchezaji wa kwanza kufunga kwa pande zote kwenye mechi ya michuano ya FIFA - na bado timuyake ikafungwa. Wachezaji sita wengine waliowahi kufanya hivyo wote timu zao walizokuwa wakizichezea zilishinda mechi zao. 


 - Matokeo ya Tahiti 1-6 Nigeria ni matokeo ya moja kati ya mechi 8 za kombe la mabara zilizozaa magoli mengi - 7.  Ni mechi moja tu ya Brazil 8-2 Saudi Arabia ndio imezidi idadi hiyo ya mabao kwa mechi. 

No comments:

Post a Comment