Search This Blog

Wednesday, June 19, 2013

KUELEKEA MECHI YA BRAZIL VS MEXICO USIKU WA LEO: HIZI NDIO TAKWIMU MUHIMU KUHUSU MCHEZO HUO - MEXICO HAIJASHINDA MECHI YOYOTE KOMBE LA MABARAA KWA MIAKA 8 SASA

Tuna masaa kadhaa ya kusubiri mechi ya pili wa kombe la mabara. Mchezo huo utakuwa dhidi ya Mexico na hizi ndio takwimu zinazohusisha mechi walizokutana magwiji hawa wa soka la bara la Amerika. 

 - Huu utakuwa mchezo wa nne kati ya Brazil-Mexico katika kombe la mabara, hivyo kuifanya mechi hii ndio ndio iliyochezwa mara nyingi zaidi katika historia ya michuano hii - mechi nyingine iliyochezwa mara nyingi ni Brazil-USA

 - Mchezo huu utakuwa wa 30 kwa Brazil katika michuano hii, ikiwa ndio timu iliyocheza mechi nyingi zaidi. 


 - Mexico wanawafuatia Brazil kwa kucheza mechi nyingi, mchezo wao wa leo utakuwa wa 21. 


 - Timu hizi mbili zimekutana mara 37, huku Seleção wakiongoza kwa ushindi wa mechi 21, wakati Mexico wameshinda mara 10.


 - Ushindi wa muhimu zaidi kwa Mexico katika hizo mara 10 ulikuwa mwaka 1999 katika kombe la mabara, ulikuwa mbele ya mashabiki wao 110,000 kwenye uwanja wa Azteca stadium


-  Mechi hii inazikutanisha timu pekee kwenye kombe la mabara 2013 ambazo zimeshashinda ubingwa wa kombe la mabara. 


 - Ushindi wa mwisho wa Mexico kwenye kombe la mabara ulikuwa siku kama ya leo - tarehe 19 June, 2005. Ni miaka 8 kamili. 

No comments:

Post a Comment