Search This Blog

Wednesday, June 19, 2013

MIAKA 125 TANGU KUANZISHWA KWA MFUMO WA LIGI KWENYE SOKA KUHADHIMISHWA KWA MECHI 6 ZA KIHISTORIA

Mfumo wa soka kuchezwa kwa ligi utatimiza misimu 125 tangu kuanza kwake kwa kuchezwa kwenye mechi 6 mwanzoni mwa ufunguzi wa ligi. 

Mechi mbili zimechaguliwa kutoka kwenye kila daraja - mechi ambazo zitahusisha baadhi ya timu ambazo zilikuwa za kwanza kuunda mfumo wa ligi msimu wa 1888-89, michezo hiyo itaanza kuchezwa kwenye wikiendi ya August 3.

Timu hizo ni Derby County ambayo itaikaribisha Blackburn Rovers wakati mahasimu Burnley na Bolton Wanderers watakutana pale Turf Moor - moja ya viwanja vitatu vya kihistoria bado kinatumika kwenye ligi ya daraja la kwanza.

Deepdale, uwanja wa nyumbani wa Preston North End, ni uwanja mwingine wa kihistoria na wataikaribisha Wolverhampton Wanderers. Utakuwa mchezo wa 2,343 wa soka la ligi kuchezwa kwenye uwanja huo - ukiwa ndio uwanja uliochezewa mechi nyingi zaidi za ligi kuliko vingine. 
Mchezo mwingine wa pili wa League One utahusisha klabu kongwe kabisa ya proffessional, Notts County, kwenda kucheza kwenye uwanja mkongwe kabisa wa kisasa, wa Sheffield United uitwao Bramall Lane.

Kwenye League Two, Newport County - timu ambayo imepanda daraja hivi karibuni kupitia Conference play-offs - watacheza na Accrington Stanley. Na mechi iliyochezwa zaidi katika historia ya mfumo wa ligi kati ya Rochdale na Hartlepool United - itachezwa kwa mara 137.


No comments:

Post a Comment