Search This Blog

Sunday, May 19, 2013

KWA STAILI YA AINA YAKE ROBERTO MANCINI AWAAGA MASHABIKI WA CITY


Siku moja ambayo gazeti la Daily Mail liliandika stori ya namna baadhi ya wachezaji wa walivyokuwa hawampendi kocha wao aliyefukuzwa Roberto Mancini, muitaliano huyo ambaye hakuachwa mpaka amalize mechi za ligi zimalizike alitumia ukurasa mzima wa gazeti la Manchester Evening kuweka tangazo la kuwaaga mashabiki liloandikwa "Manchester City supporters 3 UNFORGETTABLE YEARS," kwenye tangazo hilo pia kuna picha ya Mancini akiaaga huku kukiwa kuna makombe matatu ya EPL, FA na Ngao ya Hisani. Pia akaandika "You will always be in my heart. Ciao. Roberto Mancini."
Mancini alikuwa akipendwa na mashabiki hata baada ya kumaliza nafasi ya pili nyuma ya Man United na kufungwa na Wigan kwenye fainali ya FA Cup. Ingawa hali ilikuwa tofauti kwa wachezaji na wamiliki ambao wote walipoteza imani nae.

No comments:

Post a Comment