Search This Blog

Monday, May 27, 2013

HIZI NDIO SILAHA ZILIZOPATIKANA KWENYE FAINALI YA COPPA ITALIA KATI YA LAZIO VS AS ROMA

Fainali ya mwaka huu ya Coppa Italia kwa mara ya kwanza imezikutanisha timu kutoka Rome, Lazio vs AS Roma hivyo timu zote zikacheza kwenye uwanja wake wa nyumbani (Stadio Olimpico ambao unatumiwa na timu hizo zote). Kutokana na mechi hiyo kuhusisha timu zenye upinzani mkali tena zikigombania kombe mamalaka za usalama walihisi kungeweza kutokea vurugu kubwa hivyo wakaimarisha ulinzi mkubwa kwenye mji huo na viunga vyote vya uwanja wa Stdio Olimpico.

Kufuatiwa ulinzi huo Polisi jijini Roma walikamata silaha nyingi ambazo zingeweza kutoa uhai wa mashabiki ambao wenye upinzani mkali kutokana na mapenzi yao kwa vilabu hivyo viwili vya mji huo - ilipatikana mishale na visu ambazo vingeweza kuharibu mchezo huo wa kihistoria.

Mchezo huo ulifanyika kwa amani na mwishowe Lazio walifanikiwa kubeba kombe la Coppa Italia kwa kuwafunga Roma 1-0, likiwa kombe la 7 la Coppa na la kwanza tangu mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment