Search This Blog

Thursday, May 9, 2013

BREAKING NEWS: EVERTON WATHIBITISHA DAVID MOYES ATAONDOKA MWISHONI MWA MSIMU - MAN UNITED BADO KIMYA

Taarifa rasmi kutoka kwa klabu ya Everton zinasema kocha David Moyes ataondoka kwenye klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.
Taarifa rasmi iliyotolewa na Everton ilisema "Everton inathibitisha kwamba David Moyes ataondoka kwenye klabu hii mwishoni mwa msimu.
"Kocha alikutana na mwenyekiti Bill Kenwright mapema jana jioni na kumwambia matamanio yake ya kujiunga na Manchester United.
"Mwenyekiti, kwa niaba ya klabu, angependa kutoa shukrani za dhati kwa David kwa mchango wake mkubwa alioutoa tangu alipojiunga nasi March 2002. Amekuwa meneja wa wa aina yake."


Wakati huo huo Manchester United bado haijathibitisha kwamba Moyes ndio kocha atakayemrithi Sir Alex Ferguson.

No comments:

Post a Comment