Search This Blog

Thursday, May 9, 2013

MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI TFF SEPTEMBA 29



Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unatarajiwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu baada ya ule wa Dharura wa marekebisho ya Katiba ulipangwa kufanyika Julai 13 mwaka huu.

Tarehe hizo zimepangwa na kikao cha dharura cha Kamati ya Utendaji ya TFF kilichofanyika leo (Mei 9 mwaka huu) jijini Dar es Salaam chini ya uenyekiti wa Rais wake Leodegar Tenga ambacho kupokea rasmi maagizo ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) na kupanga utekelezaji wake.

“Kamati ya Utendaji ya TFF imepokea rasmi barua ya FIFA na kupanga utekelezaji wake. Tumepokea maagizo ya FIFA yanayotuelekeza cha kufanya, si TFF wala mtu mwingine yeyote anayeweza kuongeza jambo lingine.

“Maagizo ni undeni Kamati ya Maadili, Kamati ya Rufani ya Maadili, fanyeni marekebisho ya Katiba, anzeni tena uchaguzi, waliokuwepo na wengine wapya waruhusiwe. Tumejitahidi kuhakikisha uchaguzi uwe kabla ya Oktoba 30 mwaka huu kama FIFA walivyotuagiza,” amesema Rais Tenga wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Amesema kazi kubwa itakuwa ni kutayarisha kanuni hizo, kwani Kamati za Maadili lazima ziwe na kanuni zake na kuhakikisha kuwa hakuna mgongano kati ya Kanuni za Nidhamu na Kanuni za Maadili.

Pia Rais Tenga amesema kuna kazi ya kuangalia jinsi zitakavyoingia katika uchaguzi ambapo maana yake muda wa mchakato wa uchaguzi utakuwa zaidi ya siku 40 za sasa, hivyo mabadiliko hayo yatagusa vilevile Kanuni za Uchaguzi.

Kwa mujibu wa ratiba ya utekelezaji, rasmu ya mwanzo ya Kanuni hizo inatakiwa iwe imetoka kufikia Mei 30 mwaka huu ambapo itapelekwa FIFA kwa ajili ya kupata mawazo yao kabla ya kuendelea na hatua inayofuata.

Juni 15 mwaka huu Kamati ya Utendaji ya TFF itakutana kupokea mapendekezo hayo ambapo baada ya kuyapitisha itayapeleka tena FIFA. Taarifa (notice) ya Mkutano Mkuu wa Dharura ambayo kikatiba ni siku 30 itatolewa Juni 12 au 13 mwaka huu.

Baada ya Mkutano Mkuu wa Dharura wa marekebisho ya Katiba, Kamati ya Utendaji itakutana kati ya Julai 14 na 15 mwaka huu kuunda Kamati ya Maadili na Kamati ya Rufani ya Maadili ili kuruhusu mchakato wa uchaguzi uanze.

3 comments:

  1. SAMAHANI LAKINI....HIVI ANGETILE BADO YUKO MADARAKANI.....?

    SHAME ON HIM....!!

    ReplyDelete
  2. Kaka Shaffih, mimi ni mdau soka, na kila siku lazima nitembelee shaffihdauda.com kujua kilichojiri kwenye sport


    Kwa habari ya Tenga niliyoisikia jana, sikumwelewa
    Katika mhundo mzima wa TTF Napenda kujua yafuatayo:
    1. Wajumbe wa kamati tendaji ya TFF ni akina nani? wao sio
    viogonzi wa TFF wa mikoa?

    2. Na hao wajumbe wa kamati tendaji ya TFF wanachaguliwa na nani ?

    3. Kwa kifupi tunaomba utuwekee utaratibu wa uendeshaji wa TFF.
    Zile kamati ambazo FIFA iliagiza ziuundwe,Wanaoziunda hizo kamati
    ni akaina nani? Tenga mwenyewe,kamati tendaji au mkutano mkuu?

    Mdau kutoka Arusha

    ReplyDelete
  3. Bado yupo,yeye ni mtaalam,yuko pale kwa kuajiriwa kutokana na shule yake na sio kwa kupigiwa kura. mkataba wake ukimalizika na wewe nenda ukachukue nafasi yake,naamini unazo sifa zaidi yake

    ReplyDelete