Search This Blog

Friday, April 19, 2013

MARIO BALOTELLI AWAFUNIKA MESSI, RONALDO NA BECKHAM KWA KUTAJWA KUWA NDIO MWANASOKA MWENYE USHAWISHI MKUBWA ZAIDI DUNIANI


Mario Balotelli amekuwa ndio mwanasoka pekee kutajwa kwenye listi ya watu mashuhuri ya jarida la Time kwa mwaka 2013. Listi hiyo ambayo iliwahi kuwaingiza wansoka kama Beckham, Drogba, Messi na wengine huko miaka ya nyuma mwaka huu wote wametoswa na mtoto mtukutu Balotelli amekula shavu la kuwemo kwenye listi hiyo ambayo imewajumuisha wasanii kama Jay Z, , Beyonce, huku wanamichezo wakiwa wanne tu Balotelli, Lebron James, Lindsey Vonn na mcheza Tennis Li Na.

Baada ya kutangazwa kwa listi hiyo gwiji wa soka wa Italia na Chelsea ambaye kwa sasa ni manager wa Watford Gianfranco Zola, alizungumzia Balotelli kwa kusema:
"Kwa mbali, watu wanaweza kudhani kichaa, lakini Mario ni kijana mzuri mwenye upendo na mcheshi. Ninakuhakikishia nimekuwa nikijisikia amani kila ninapokutana nae. Amerudi Italia akitokea England akiwa kama mshindi huku akiwa na nyota ya mvuto. Sasa anapaswa kutulia na kuwa mfano bora, anapenda presha, lakini ili kufanikiwa inabidi ajue namna ya kuidhibiti." Alisema Zola.

No comments:

Post a Comment