Search This Blog

Friday, April 19, 2013

MCHEZAJI ANAYECHEZEWA FAULO ZAIDI BARANI ULAYA MSIMU HUU - SIO MESSI WALA RONALDO - NI DIAMANTI

Hakuna shaka kwamba Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wamekuwa wakichezewa rafu sana timu pinzani dimbani, lakini hakuna hata mmoja kati yao anayefikia kuwa mchezaji ambaye anafanyiwa madhambi mengi kuliko brani ulaya msimu huu. 

Kwa mujibu wa kampuni inayokusanya data za kimichezo ya Opta, mchezaji anayechezewwa rafu nyingi kuliko wote ndani ya bara la ulaya msimu huu ni kiungo wa timu ya Serie A  Alessandro Diamanti.

Kama takwimu zinavyoonyesha hapo chini Diamanti amechezewa faulo mara 123 msimu huu, wakati Messi na Ronaldo wakiwa wamechezwa faulo mara zisizozidi 75 kila mmoja. Kiufupi wachezaji hawa wanaotajwa kuwa bora ulimwenguni kwa sasa hawapo hata kwenye top 5. Mchezaji wa Wolfsburg Diego ndio mchezaji mwingine ambaye kidogo anamsogolea Diamanti akichezewa rafu mara 100, wakati kiungo mwenye miaka 36 Francesco Totti akishika nafasi ya nne. 

 LISTI KAMILI YA WACHEZAJI WANAOCHEZEWA RAFU ZAIDI BARANI ULAYA MSIMU HUU


 Diamanti, mwenye miaka 29 kwa sasa alicheza msimu mmoja pale West Ham mwaka juzi, amekuwa kwenye kiwango kizuri kwa timu yake ya Bologna, huku akifanikiwa kuitwa timu ya taifa ya Italia iliyoshiriki Euro 2012 na kufika fainali.


)

No comments:

Post a Comment