Search This Blog

Friday, April 19, 2013

HATIMAYE LIONEL MESSI ATUMA JEZI YAKE KWA PAPA FRANCIS - ANGALIA NAMNA ILIVYOPOKELEWA NA PAPA MWENYEWE

Wote ni raia wa Argentina. Wote wanapenda mchezo mzuri. Na sasa wote wanamiliki jezi ya mchezaji bora wa dunia Lionel Messi.

Imerekodiwa video kwenye maeneo ya Vatican juzi Jumatano ikimuonyesha Padri wa Vatican akimkabidhi Papa mpya wa kanisa katoliki - Papa Francia jezi iliyosainiwa na Messi wakati wa mkutano mkuu wa kwanza wa Papa huyo mpya na wana Vatican.

Baada ya kubusu mikono ya kiongozi wake, padri Miguel Delgado Galindo alimkabidhi Pope Francis jezi ya Messi ambayo ilionekana kumfarahisha sana kiongozi huyo mpya wa kanisa katoliki duniani. 

Hii ilikuwa jezi ya pili ya timu ya soka ambayo Papa aliipokea ndani ya wiki hii, baada ya waziri mkuu wa Spain Mariano Rajoy kumkabidhi Papa Francis jezi ya Hipania mapema wiki hii.

VIDEO

No comments:

Post a Comment