Search This Blog

Saturday, April 13, 2013

MABAO 340 YATINGA NYAVUNI LIGI KUU 2012/13 - YANGA NA AZAM VINARA WA MABA0 - AFRICAN LYON NA TOTO WAONGOZWA KWA KUFUNGWA MABAO MENGI

Mabao 340 yamefungwa kwenye mechi 307 katika Ligi Kuu Tanzania iliyoanza kutimka rasmi Septemba 20, mwaka jana na kutarajiwa kufikia tamati Mei 18, mwaja huu.
Kwa idadi ya mabao hayo ni sawa na wastani kila mechi ya ligi linafungwa goli moja.
Azam FC ni timu ambayo imethibitisha kuwa na safu kali ya ufungaji mabao huku ikifuatiwa na vinara Yanga.
Wawakilishi hao pekee wa nchi katika mashindano ya kimataifa, Azam wamezamisha mabao 39 katika mechi 22 walizocheza huku Yanga ikipachika 37 kwa michezo yake 21.
Timu tatu, African Lyon, JKT Ruvu na Toto African ambazo zipo kwenye hatari ya kushuka daraja zinaongoza kwa kufungwa mabao mengi.
Lyon imeruhusu mabao 35 kutinga kwenye nyavu zake wakati JKT Ruvu ikifungwa 34 na Toto African ikifungwa 33. 

No comments:

Post a Comment