Search This Blog

Saturday, April 13, 2013

LIVE MATCH CENTRE: YANGA SC 3 - 0 JKT OLJORO


Dk 90+5 MPIRA UMEISHA! YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 90 Mpira umeongezwa dakika 5.

Dk 90 Mpira umeongezwa dakika 5.

Dk 87 Nizar Khalfan anapiga shuti kali langoni kwa Oljoro lakini kipa Shaibu Issa anapangua na kuutoa nje mpira. YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 82 Bahanunzi anachezewa vibaya kwa kutegwa mguu ndani ya eneo la hatari la Oljoro lakini mwamuzi anapeta.

Dk 78 Yanga inafanya mabadiliko, ametoka Msuva ameingia Nizar Khalfan. YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 75 Mpira umechangamka kidogo timu zote zinamiliki mpira kwa zamu.

Dk 71 Frank Domayo wa Yanga anamchezea rafu Sixbert Mohamed.

Dk 67 Oljoro inafanya mabadiliko, ametoka Karage Mgunda ameingia Sixbert Mohamed. YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 59 Majaliwa Sadik wa Oljoro ameonyeshwa kadi ya njano na mwamuzi Amon Paul wa Mara baada ya kumchezea vibaya Msuva.

Dk 58 Yanga inafanya mabadiliko, ametoka Kavumbagu ameingia Said Bahanunzi. YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 55 Emmanuel Memba wa Oljoro anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea rafu Niyonzima.

Dk 53 Niyonzima anapiga shuti kali katika lango la Oljoro lakini kipa Shaibu Issa anapangua. Issa anaumia na kutibiwa baada ya kugongana na Kavumbagu.

Dk 50 Oljoro wanafanya mabadiliko, kipa Lucheke Musa anatoka anaingia Shaibu Issa.

Dk 46 Chuji anachezewa rafu na Paul Nonga wa Oljoro.

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA
Dk 45 HALF TIME! YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 43 GOOO....! Hamis Kiiza anaipatia Yanga bao la tatu baada ya kuiwahi pasi iliyopenyezwa kutoka katikati ya uwanja na kumchambua kipa. YANGA 3-0 OLJORO.

Dk 42 David Luhende wa Yanga anatengewa mpira mzuri na Chuji lakini shuti lake linatoka nje.

Dk 36 Msuva wa Yanga anapokea pasi safi ya Nsajigwa na kupiga krosi safi ambayo ilibaki kidogo mpira uingie wenyewe golini.

Dk 32 Yanga inafanya mabadiliko, ametoka Juma Abdul ameingia Shadrack Nsajigwa.

Dk 30 Abdul wa Yanga ametibiwa na kurudi uwanjani lakini anaanguka akiwa peke yake huku akigugumia maumivu ya kifundo cha mguu. Shadrack Nsajigwa anapasha misuli moto.

Dk 24 Didier Kavumbagu wa Yanga anashindwa kuunganisha krosi safi ya Msuva kutoka wingi ya kulia.

Dk 21 Cannavaro anaumia baada ya kugongana mchezaji wa Oljoro. Mpira unasimama kwa muda na Cannavaro anatibiwa.

Dk 19 GOOO...! Msuva anaifungia Yanga bao la pili baada ya kuipangua ngome ya Oljoro na kupiga shuti hafifu. YANGA 2-0 OLJORO

Dk 16 Oljoro wanaonekana wamezinduka nao wameanza kutawala kiungo huku wakicheza pasi fupi fupi.

Dk 13 Paul Nonga wa Oljoro anatengewa mpira vizuri na Idd Swaleh lakini shuti lake linatoka nje ya lango la Yanga.

Dk 10 Yanga imetawala mchezo hasa kiungo na imefanya mashambulizi mengi langoni kwa Oljoro.

Dk 5 GOOO....! Nadir Haroub 'Cannavaro' anaipatia Yanga bao la kwanza kwa kichwa akiunga mpira wa kona. YANGA 1-0 OLJORO

3 Simon Msuva wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa Oljoro kipa anaupangua na kuwa kona. Kipa anaumia baada ya kuucheza mpira huo. Mchezo unasimama ili kipa atibiwe.

Dk 1 Juma Abdul wa Yanga anapiga shuti kali langoni kwa JKT Oljoro lakini kipa Lucheke Musa anaudaka mpira. Abdul alipewa pasi na Frank Domayo.

Dk 00 MPIRA UMEANZA!

Young Africans line-up to face JKT Oljoro today
1.Ally Mustafa 'Barthez'
2.Juma Abdul
3.David Luhende
4.Nadir Haroub 'Cannavaro'
5.Kelvin Yondani
6.Athuman Idd 'Chuji'
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo 'Chumvi'
9.Didier Kavumbagu
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Yusuph Abdul
2.Shadrack Nsajigwa
3.Oscar Joshua
4.Salum Telela
5.Nurdin Bakari
6.Nizar Khalfani
7.Said Bahanuzi


JKT Oljoro: Lucheke Musa, Yusuf Machogoti, Majaliwa Sadiki, Nurdin Mohamed, Shaibu Nayopa, Salim Mbonde, Karage Mgunda, Emmanuel Memba, Paul Nonga, Idd Swaleh na Hamis Salehe.

4 comments:

  1. Tupe na list ya Oljoro!...

    ReplyDelete
  2. Hivi simba wameshalipeleka kombe Jangwani ama bado wanalo tu.Walitangulize haraka

    ReplyDelete
  3. Uko vizuri kwenye kutoa updates,lakini jaribu kuweka picha zinazoendana na wakati>Picha iliyopo haiendani na Mechi ya jana.Gumbo,Shamte hawapo Yanga kwa sasa na Omega Seme hakuwepo kabisa.Otherwise kazi nzuri kaka,big up

    ReplyDelete