Search This Blog

Tuesday, April 23, 2013

JE WAJUA :SIO WACHEZAJI WOTE WA MAN UNITED WA KIKOSI CHA KWANZA WATAPEWA MEDALI ZA UBINGWA WA 20?

Usiku wa kuamkia leo Manchester United imeweza kutwaa ubingwa wa 20 wa ligi kuu ya England baada ya kuifunga Aston Villa kwa mabao 3-0.

Lakini Manchester United hawakupewa kikombe leo hii wakisubiri mpaka mechi ya mwisho ya nyumbani dhidi ya Swansea ndio wakabidhiwe kombe lao pamoja na medali zao za ushindi wa Barclays Premier League

Katika kikosi cha kwanza Manchester United msimu huu karibia wachezaji wote wamecheza mechi zaidi ya 10 za Premier League kasoro Nick Powel na Alexander Butner ambao hawajatimiza michezo 10 na hata kama wakicheza mechi zote zilizobakia hawatoweza kutimiza idadi ya mechi hizo ili waweze kuwa miongoni mwa wachezaji wa United watakaokabidhiwa medali baada ya mechi ya Swansea.

Sheria za Premier League kuhusu wachezaji watakaoweza kupewa medali zinasema

Mchezaji anatakiwa awe amecheza mechi zisizopungua 10 kwa klabu yake husika ili aweze kufuzu kupata medali ikiwa timu yake itachukua ubingwa.

Aidha klabu husika inaweza kutuma maombi ya medali za ziada kwa ajili ya wachezaji ambao hawakufikia idadi ya mechi 10.

2 comments: