Search This Blog

Saturday, April 6, 2013

HUKU MJI WA MANCHESTER UKIGAWANYIKA KWA RANGI 2 - HOTELI MOJA YAFANYA MAKUBWA YAANDA VYUMBA VYENYE KUMBUKUMBU, VITU NA MAJINA YA KIHISTORIA YA UNITED NA CITY

Huku muda ukizidi kusogea kuelekea mchezo wa mahasimu wa jiji la Manchester siku ya Jumatatu, mji wenyewe umekuwa katika hali ya kujigawanya kwenye rangi mbili bluu na nyekundu kama inavyokuwa kila mchezo huu unapokaribia. Ingawa safari hii mbio za ubingwa zikiwa zimekaribia kuisha na kufikia tamati.
Na wale washabiki wa timu hizi ambao watakuwa wanatoka sehemu nyingine tofauti na Manchester wametaarishiwa Hotel ya Piccadilly's Premier Inn ambao itakuwa imegawanyika kwa floors mbili tofauti zenye rangi nyekundu na bluu.
Wakati baa za katikati ya mji zikiwa tayari zina himaya aidha ya United au City, hotel hiyo iliyopo maili kadhaa kutoka uwanja wa Old Trafford imechukua njia tofauti kuwapa hali washabiki watakaofikia hotelini kwa ajili ya mchezo husika.

Wameandaa vyumba vilivyopewa kumbukumbu na watu muhimu wa vilabu hivyo viwili vya mji wa Manchester.
 
 
Late check-in: City fans can remind themselves of the greatest moment in their history
Chumba hiki ni maalum kwa washabiki wa Man City kujikumbusha muda ambao Aguero alipofunga goli la ushindi ya QPR na kuipa City ubingwa msimu uliopita.


Red carpet
Upande huu ni washabiki wa United
Blue carpet
Hii sehemu ya vyumba vya washabiki wa Man City

Mashabiki wa United wametaarishiwa vyumba vyenye majina kama vile fans  Room 99 - 'The Treble Room' - and Room 19 - 'The Champions Suite' - ili kuwapa hali ya kwenda kuipa nguvu timu yao waweze kujihakikishia ubingwa mwingine wa 20 wa kihistoria katika Premier League .

Kwa upande wa japokuwa baadhi wameanza kukata tamaa ya ubingwa msimu huu wametaarishia chumba cha kujikumbusha ubingwa wao kwa kukumbuka muda wa goli la Aguero lilowapa ubingwa kwa chumba kimojawapo kupewa jina la "The Aguero Suite' in room '93:20'.


 Wakati mashabiki ambao hawashabikii upande wowote baina ya timu hizo mbili wamepewa chumba kilichopewa jina la watu waliozitumikia timu zote mbili  'Dennis Law Suite' na 'The Sparky Mark Hughes Suite', 




2 comments:

  1. wenzetu wakali, nmekubal they know what they are doing, biashara bhana! itabid hii tech. tuwape wachaga na waking ndo wanajua biashara

    ReplyDelete
  2. Keneth asamoah suite 119:29
    (kagame Cup)

    ReplyDelete