Search This Blog

Thursday, April 25, 2013

GARY NEVILLE AIOKOA TIMU YA MTAANI KWAO KUFILISIKA - ALIPA MISHAHARA YA WACHEZAJI

Nahodha na mchezaji wa zamani Man United  Gary Neville amesaidia kulipa mishahara ya klabu ya nyumbani kwao inayokabiliwa na ukata mkubwa.

Bury FC — ambayo imeshuka daraja hivi karibuni mpaka ligi daraja la pili — inahitaji kiasi cha £1million ili kijihakikishia uwepo wake.
Klabu hiyo itashindwa kuendelea kuwepo mpaka pale watakapopata wafadhili wa kuwasaidia.
Gary Neville ambaye kwa sasa kocha msaidizi wa England na mchambuzi wa soka wa TV, aliingia mfukoni mwake na kuamua kulipa mishara ya wachezaji wote baada ya kuombwa na klabu hiyo.


No comments:

Post a Comment