Search This Blog

Friday, March 8, 2013

SALUM MACHAKU: NASHANGAZWA NA SIMBA INAVYOFANYA VIBAYA

WINGA wa zamani wa Simba, Salum Machaku amesema anashangazwa na timu hiyo kufanya vibaya kwenye michezo yake mbalimbali hivi karibuni.
Machaku anayechezea Polisi Morogoro alisema Simba ina kikosi kizuri na benchi la ufundi limejaa watu makini, lakini wanashindwa kufanya vizuri.
"Sidhani kama benchi la ufundi ni baya kiasi hicho, labda kuna matatizo mengi ya ndani yanayoichanganya Simba.
Machaku ambaye akutaka kuzungumzia kwa undani juu ya hali ya klabu yake zamani, lakini anaamini kocha Mfaransa Patrick Liewing ni moja wa makocha bora ni hivyo anatakiwa kupewa nafasi zaidi kwenye kukinoa kikosi hicho.
Akizungumzia kikosi chake cha Polisi Morogoro winga huyo alisema kinachotakiwa sasa ni kuhakikisha wanashinda kila mechi ili waweze kujiweka katika mazingira mazuri ya kutoshuka daraja msimu huu.

No comments:

Post a Comment