Search This Blog

Saturday, March 9, 2013

LIVE MATCH CENTRE: YANGA 1 - 0 TOTO AFRICA FULL TIME







Dk 90+4 FULL TIME. YANGA 1-0 TOTO

Dk 90 Toto imefanya mabadiliko ametoka Musa Musa, ameingia Simba Boaz.

Dk 88 Kiiza anafunga bao lakini mwamuzi anakataa kwa kuwa ni off side.

Dk 85 Kiiza anaonekana anataka kufunga tu, kila mpira anaoupata hatulii nao anaupiga langoni kwa Toto.

Dk 82 Kiiza anakosa bao la wazi akiwa amebaki peke yake na kipa wa Toto.

Dk 78 GOOOO....! Nizar Khalfan anaipatia Yanga bao la kwanza akiunganisha krosi ya Kiiza. Mpira uliopigwa na Nizar ulimparaza kipa wa Toto, Ngwegwe na kutinga wavuni. YANGA 1-0 TOTO.

Dk 74 Kavumbagu anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Swita wa Toto. YANGA 0-0 TOTO

Dk 73 Yanga imefanya mabadiliko, ametoka Godfrey Taita ameingia Didier Kavumbagu.

Dk 67 RED CARD...! Eric Mlilo wa Toto anaonyeshwa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya Msuva. Mlilo alikuwa na kadi ya njano awali, hivyo mwamuzi amemwonyesha kadi ya njano kisha nyekundu.

Dk 64 Yanga inafanya mabadiliko, ametoka Tegete ameingia Nizar Khalfan.

Dk 62 Toto imefanya mabadiliko, ametoka Chika Olugbe, ameingia Simba Boaz.

Dk 60 Toto imefanya mabadiliko, ametoka Severine Constantine, ameingia Heri Mohamed.

Dk 57 Msuva anakosa bao baada ya mpira wa kichwa alioupiga akiunga krosi ya Kiiza, kudakwa na kipa wa Toto, Eric Ngwegwe.

Dk 53 Mshika kibendera Abdallah Mkomwa wa Pwani anaipa Yanga penalti baada ya Msuva kupambana na beki Eric Kyaruzi wa Toto. Mwamuzi Andrew Shamba ameikataa penalti kwa kile kinachooneka kwamba beki wa Toto alicheza mpira na hakumgusa Msuva.

Dk 51 Jerry Tegete wa Yanga anakosa bao la wazi akishindwa kuunga vyema krosi ya Kiiza.

Dk 49 Katika kiungo leo hapa uwanjani kuna mchuano mkali kati ya Swita wa Toto na Niyonzima wa Yanga. YANGA 0-0 TOTO.

Dk 46 Hamis Kiiza anakosa bao la wazi baada ya kupewa pasi nzuri na Frank Domayo. Kiiza raia wa Uganda anajiangusha na kushindwa kupiga mpira.

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA.

Dk 45 HALF TIME. YANGA 0-0 TOTO.

Dk 43 Swita wa Toto anamchezea rafu Haruna Niyonziama wa Yanga na anaonyeshwa kadi ya njano. Niyonzima anamvamia Swita baada ya kukerwa na rafu hiyo. Swita amewahi kuichezea Yanga.

Dk 39 Beki wa Toto, Evarist Maganga anagongana na Hamisi Kiiza wa Yanga na kuumia. Anatibiwa na kuendelea na mchezo.

Dk 33 Mbuyu Twite wa Yanga anayecheza kama beki wa kati leo, anamchezea vibaya Emmanuel Swita wa Toto.

Dk 30 Simon Msuva wa Yanga anapoteza mpira jirani na lango lake, Hamis Msafiri wa Toto anaunasa mpira na kupiga shuti kali linalotoka nje kidogo ya lango la Yanga.

Dk 25 Mpira ni kawaida mno, kila timu zinafanya makosa mepesi hasa wachezaji kupoteza mipira na pasi nyingi hazina macho.

Dk 20 David Luhende wa Yanga anamchezea rafu Musa Musa wa Toto. YANGA 0-0 TOTO

Dk 16 Hamis Kiiza anaifungia Yanga bao la kichwa akiunga krosi ya Godfrey Taita, lakini mwamuzi Andrew Shamba wa Pwani anakataa kwa kuwa mfungaji alimchezea vibaya kipa kabla ya kufunga.

Dk 7 Eric Mlilo wa Toto anamchezea rafu David Luhende wa Yanga.

Dk 5 Mpira bado haujatulia lakini Toto African ndiyo waliofika mara nne langoni kwa Yanga. Yanga imefika mara mbili langoni kwa Toto.

Dk 2 Uwanjani kuna mvua, mashabiki ni wachache na pitch inatereza kiasi japokuwa hali ya uwanja ni nzuri.

00 MPIRA UMEANZA!

Young Africans line-up to face Toto Africans today:
1.Ally Mustafa
2.Godfrey Taita
3.David Luhende
4.Mbuyu Twite
5.Kelvin Yondani
6.Athumani Idd
7.Saimon Msuva
8.Frank Domayo
9.Jerson Tegete
10.Hamis Kiiza
11.Haruna Niyonzima

Subs:
1.Said Mohamed
2.Shadrack Nsajigwa
3.Oscar Joshua
4.Omega Seme
5.Nizar Khalfani
6.Said Bahanuzi
7.Didier Kavumbagu

Toto Line Up: Eric Ngwegwe, Eric Mlilo, Robert Magadula (C), Eric Kyaruzi, Evarist Maganga, Hamis Msafiri, Severine Constantine, Emmanuel Swita, Chika Olugbe, Musa Musa na Mohamed Jingo.

No comments:

Post a Comment