Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

PELE: "NEYMAR NI MCHEZAJI WA KAWAIDA ANAPOKUWA NDANI YA JEZI ZA BRAZIL"

Pele
 
 
Brazil imeweka majukumu mazito kwenye mabega ya kinda la nchi hiyo Neymar na mchezaji huyo anakuwa wa kawaida anapoiwakilisha nchi yake, amesema mfalme wa soka duniani Pele. 

Neymar, ambaye anaichezea Santos timu ambayo Pele aliichezea kwa zaidi ya nusu ya maisha yake ya soka, amekuwa akitajwa mchezaji bora kuwahi kutokea nchini Brazil katika miaka ya hivi karibuni na anategemewa kuiongoza Brazil kwenye kombe la dunia 2014.

Lakini wachambuzi wanasema anakosa uzoefu dhidi ya mabeki wa daraja la dunia na anahitaji kujikaza na kupambana vizuri na sio kujiangusha angusha kutafuta free kicks.
 
"Kuna kumtegemea sana Neymar lakini anakuwa mchezaji wa kawaida anapoichezea Brazil," Pele aliiambia gazeti la Estado de Sao Paulo kwenye mahojiano. 

"Kila kitu kinamzunguka Neymar, lakini ni mchezaji ambaye hana uzoefu wa kwenye ngazi ya kimataifa." 

"Ni mchezaji mzuri lakini hana uzoefu wa kucheza nje ya mipaka ya Brazil. Kila mtu anafikiria ataweza kutoa suluhisho la matatizo ya timu ya Brazil lakini hajajiandaa kuubeba mzigo huo," aliongeza mshindi huyo wa kombe la dunia kwa mara ya tatu. 

Huku akiwa na mikataba 11 ya udhamini kuiangalia, kumekuwepo na hali ya kutokueleweka kuhusu maisha ya nje ya uwanja ya Neymar. 

"Hachezi nje ya nchi na soka la ulaya. Pale Santos, wanasema ni mchezaji bora duniani lakini ananipa wasiwasi kuhusu tabia yake ya kuwa hodari kwenye kutokea kwenye vyombo vya habari kuliko alivyo uwanjani," alisema Pele.

"Anapenda kupata free kicks nyepesi .... michezo ni migumu nchini England, Italy, Germany. Marefa huwa hawana tabia ya kupiga filimbi ovyo ovyo. 

Mshambuliaji huyo mwenye miaka 21 alipata kadi yake nyekundu ya tano kwenye maisha yake ya soka kwenye mechi waliyofungwa na Ponte Preta wikiendi iliyopita. 

Pele alisema Neymar huwa anajaribu kufanya vitu vingi sana anapoichezea klabu yake.

"Free kicks zote, penati, na kona zinapigwa na Neymar. Kila mara anapopiga free kick, ina maana anakuwa nje ya mchezo kwa karibia dakika moja.

"Anatumia muda mwingi nje ya mchezo.....inabidi awe nje ya box la penati, akusanye mipira na kutumia ujuzi wake wa kuuchezea kusababisha madhara kwa wapinzani."

No comments:

Post a Comment