Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

GALATASARY KUTOKA KWENYE DIMBWI LA MADENI MPAKA KUWA KLABU TAJIRI - FUNZO KWA VILABU VYA SIMBA NA YANGA



Mnamo mwaka 2011, Unal Aysal alichaguliwa kuwa Raisi mpya wa Galatasaray, klabu ambayo wakati huo ilikua na deni linalozidi euro milioni 240.
Kwa kifupi klabu ilikuwa ni kama mufilisi.
Tangu Unal Aysal alipoichukua timu takribani miaka miwili iliyopita Galataray mambo yake kiuchumi yanakwenda vizuri, kwasasa wanashika nafasi ya 30 kwenye msimamo wa vilabu tajiri ulimwenguni.

Baadhi ya wanasoka mahiri ulimwenguni kama vile Didier Drogba na Wesley Sneijder wamevutiwa na Gala inayoutumia uwanja mpya wa kisasa wa Turk Telekom pamoja na wachezaji wengine wenye majina kama Fernando Muslera, Emmanuel Eboue, Johan Elmander na Burak Yilmaz.

Namna gani mambo yamebadilika ghafla bin vuu?

Jibu jepesi la mafanikio ya Galatasary ni jina la mmiliki wa timu hiyo ndugu Aysal, tajiri anayeshika nafasi ya 45 kwenye orodha ya matajiri nchini Uturuki, aliutumia utajiri wake kutatua matatizo lukuki yaliyokuwa yanaikabili Gala kama ambavyo Abramovich alifanya kuinusuru chelsea. 

Aysal aliwekeza kwa wachezaji wapya mara tu baada ya kuwasili pamoja na kumuuza aliyekuwa nahodha  Arda Turan kwenda Atletico Madrid, aliwasajili wachezaji kama golikipa wa timu ya taifa ya Uruguay  Muslera, Eboue, Elmander na Felipe Melo.

Uwekezaji huo ulilipa mara moja kwani Galatasaray walishinda ubingwa wa Uturuki, ubingwa uliowaingizia kitita cha euro milioni 30m, kwa kufuzu tu kwenye michuano ya Uefa champions league pia waliweka kibindoni kiasi cha euro milioni 27. Kufunguliwa kwa uwanja mpya wa Turk Telekom Arena wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 52,000 wakiwa wameketi vitini walifanikiwa kuingiza kiasi kingine cha Euro milioni 30 kutokana na VIP lounges pamoja na ununuzi wa tiketi za msimu.

Sehemu ya utata kwenye deals za biashara za Galatasaray ilionekana kwenye soko la hisa . Kati ya mwezi agosti na mwezi desemba mwaka 2011, waliuza asilimia 28.35 ya hisa za klabu toka kwenye kampuni mama ya Galatasaray AS deal ambayo iliingizia klabu euro milioni 70 .

Hii ilifuatiwa na tangazo kuwa mapato yote ya mlangoni kwenye uwanja wa Turk Telkom Arena yataenda moja kwa moja kwenye tawi la soka la timu hiyo  kinyume na ilivyokuwa awali chini ya kampuni mama ambayo iliingiza sehemu ndogo ya mapato kwneye maendeleo ya timu.
Kisha likaja ongezeko la asilimi 400% la hisa za kampuni ongezeko ambalo lilishusha thamani ya wana hisa binafsiambao walilazimika kulipa euro 11 kwa kila hisa jambo ambalo liliongeza mapato na kufikia idadi ya euro milioni 117. Kinyume na ilivyo kawaida, klabu haikulipa faida kwa wanahisa kama inavyohitajika faida ya euro 65 bali iliandika toka kwenye makato ya mlangoni ya mechi za usoni .

Miezi mitano baadaye kampuni iliripoti ongezeko la asilimia 300% kwenye hisa za msingi, jambo ambalo bodi maalum ya uangalizi wa masuala ya biashara ilizuia .

Kubalance mahesabu ilikuwa sehemu ya mpango mkubwa wa kuifanya Gala kuwa kampuni inayofanya vizuri kibiashara . Mfano mzuri ni usajili wa Drogba na Sneijder ambao wamesajiliwa kwa malengo ya kuleta ushindi uwanjani na upande wa biashara huku kodi zao zikilipwa na watu wengine.
CEO wa kampuni inayomiliki Galatasaray amesema kuwa lengo ni kutwaa ubingwa wa ligi ya Uturuki na kufanya vizuri Ulaya na kuifanya Gala kuwa klabu bora ulimwenguni. Hilo linaendana na kauli ya mkurugenzi huyo ambaye amesema kuwa klabu hiyo inahitaji wachezaji wakubwa ili kutimiza malengo makubwa.
Wakati Gala walipotwaa kombe la UEFA mwaka 2000 , mishahara ya Gheorge Hagi, Gheorge Popescu, Claudio Tafarrel na wengine ilileta balaa katika miaka iliyofuatia hali iliyosababisha kikosi kupunguzwa na hili liko hatarini kutokea kwa sasa.
Jinsi ya kutatua tatizo hili Aysal anasema kuwa falsafa yake kama mfanyabiashara anaamini kuwa mfanyabiashara anapaswa kuwa mtu mwenye uthubutu, na mbishi. Kwake kuwa mbahili hakukufanyi uwafurahishe mashabiki na kuuza tiketi.
Mashabiki kwa sasa wana furaha, na Aysal anaamini kuwa Gala itakuwa klabu kubwa duniani siku si nyingi na hili ni jambo ambalo mashabiki wa Fernabace na Besiktas wanacheka wakilisikia. Ila hawacheki wakiona Gala inawapanga Drogba na Sneijder kwenye mechi zao huku wakijiandaa kucheza 16 ya Ligi ya mabingwa.
Kamari aliyocheza Aysal inaonekana kulipa ila lazima klabu ishinde nyumbani na ulaya ili kuepuka historia ya kina Hagi na Tafarel kujirudia .

No comments:

Post a Comment