Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

MILOVAN KULIPWA FEDHA ZAKE ANAZOIDAI SIMBA NA MALKIA WA NYUKI NDANI YA KIPINDI CHA WIKI

MWENYEKITI wa Kamati ya Utendaji ya Simba, Rahma Al Kharusi ameahidi kumlipa aliyekuwa kocha wa timu hiyo Milovan Cirkovic dola 32,000 ambazo anaidai klabu hiyo.

Milovan anaidai Simba fedha hizo kutokana na kuvunjwa kwa mkataba, malimbikizo ya mshahara miezi mitatu iliyobaki pamoja na mshahara wa mwezi mmoja.

Al Kharusi alimwalika Milovan raia huyo wa nchini Serbia na kuzungumza naye kwa kirefu juu ya madai yake kwa Simba katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kharusi ambaye ameondoka jana kurejea Oman alisema:

"Nitamlipa Milovan (Cirkovic) fedha zake zote ambazo anaidai Simba kabla ya Jumatano ijayo.

Alisema yeye haogopi chochote na anasema kitu ambacho anakiona hakifai ndani ya uongozi wa timu hiyo.

"Kwa sababu sitaki kuona ubabaishaji nitasema jambo lolote ambalo naliona halina mashiko na timu."

"Unajua ni kitu cha ajabu, kocha huyu tunaweza kumwitaji baadaye, kwa hiyo si vizuri kumchosha,"alisema Al Kharusi.

Akizungumzia pambano la Simba na Libolo Ligi ya Mabingwa alisema; "Timu haikucheza vizuri kabisa naona kama walikuwa wanafanya mazoezi."

No comments:

Post a Comment