Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

KOCHA WA STARS ASEMA ATAENDELEA KUKITUMIA KIKOSI CHAKE KILE KILE MECHI YA MOROCCO


KOCHA wa Taifa Stars, Kim Poulsen amesema hakuna uwezekano wa yeye kuita wachezaji mpya katika kikosi chake kitakachokabiliana na Morocco.

Stars itacheza na Morocco Machi 22 Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kusaka tiketi yakushiriki fainali za Kombe la dunia zitakazofanyika Brazil mwakani.

Akizungumza jijini Dar es Salaam Kim  alisema sababu kubwa yakutofikiria kongeza mchezaji mpya kwenye kikosi hicho ni muda mchache wa timu hiyo kujiandaa na kabla ya mchezo huo.

"Sifikiri kuongeza mchezaji mpya kwakua muda wa kujiandaa ni mchache mno."

Alisema; "Ligi inaendelea na wachezaji wanatumikia klabu zao, hii ina maana pengine nitatumia siku nne au tano kukaa kambini na wachezaji."

"Sina maana mbaya isipokuwa muda wa kujiandaa ni mdogo mno. Nilipenda sana kuongeza mchezaji mpya katika safu ya ulinzi na kiungo, lakini siwezi kufanya hivyo tena."

Stars imeshinda mechi mbili za kirafiki dhidi ya Zambia na Cameroon kwa idadi ya bao 1-0 kila mechi.

1 comment: