Search This Blog

Wednesday, February 20, 2013

LIVE MATCH CENTRE: AZAM 4 - 0 JKT RUVU - SIMBA 1 - 0 PRISONS FULL TIME


 DK 45 za kipindi cha pili zinaisha hapa uwanja wa Sokoine na Simba inaondoka na ushindi umuhimu kujaribu kukimbizana na wapinzani wao walioko juu yao Azam na Yanga.

 DK 40: Kipindi cha pili kinaelekea mwishoni na Simba inaendelea kuongoza 1-0 dhidi ya Prisons.

 Kutoka Sokoine Mbeya - DK 70 - Simba wanaendelea kuongoza lakini wanashambuliwa sana na Prisons.

Chamazi: AZAM FC 4 - 0 JKT RUVU

 Dk 90 Mwamuzi anaongeza dakika nne za nyongeza. JKT wanachangamka kidogo na kuliandama lango la Azam. JKT  0-4 AZAM.

Dk 86 Azam inaendelea kutawala mchezo hasa kiungo na kufanya mashambulizi kadhaa langoni kwa JKT. JKT 0-4 AZAM.

Kutoka Mkwakwani: Coastal 2 - 0 JKT Oljoro

 Dk 81 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Ibrahim Mwaipopo ameingia Gaudence Mwaikimba. JKT 0-4 AZAM.

Dk 76 Kocha wa Yanga, Ernie Brandts na msaidizi wake Fred Minziro wanaondoka uwanjani baada ya kuitazama Azam ambaya watacheza nayo Jumamosi hii katika muendelezo wa Ligi Kuu ya Bara. JKT 0-4 AZAM.

Dk 72 Gooo....! Abdi Kasim 'Babi' anaipatia Azam bao la nne kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya Seif Abdallah. Babi anafunga bao hilo akiwa anagusa mpira wa kwanza tangu aingie dakika moja iliyopita. JKT 0-4.

Dk 71 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Bocco ameingia Abdi Kasim. JKT 0-3 AZAM.

Dk 70 JKT inafanya mabadiliko, ametoka Amos Mgisa ameingia Emmanuel Pius.

Kutoka Mbeya - Sokoine - Kipindi kinaanza na Simba wanaendelea kuongoza 1 - 0 

 Dk 67 Azam inafanya mabadiliko, ametoka Kipre Tchetche ameingia Seif Abdallah. JKT 0-3 AZAM.

Dk 60 JKT inafanya mabadiliko, wametoka Kisimba Luambano na Mussa Mgosi, wameingia Hussein Dumba na William Sylevester.

 Dk 54 Kipa wa JKT, Shaaban Dihile anaumia baada ya kuokoa mpira wa shuti kali lililopigwa na Mcha. Mpira unasimama kwa muda ili Dihile atibiwe.

Dk 51 JKT wanacharuka na kupanga mashambulizi lakini safu ya ulinzi ya Azam inaonekana kuwa makini na kuokoa hatari zote.

Kutoka Mbeya Soine Stadium - Simba inaongoza kwa bao moja lilofungwa na Amri Kiemba kwenye dakika ya 26 kipindi cha kwanza. Sasa hivi ni kipindi cha kwanza kinaendelea.

 Dk 46 Gooo...! Mcha anaipatia Azam bao la pili kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya Bocco. JKT 0-3 AZAM.

Dk 45 KIPINDI CHA PILI KIMEANZA. JKT 0-2 AZAM.

Dk 45 HALF TIME! JKT 0-2 AZAM.

Dk 45 Gooo....! John Bocco anaipatia Azam bao la pili akiunganisha pasi ya Humphrey Mieno. JKT 0-2 AZAM.

Dk 42 Samwel Kamuta wa JKT anapiga shuti kali langoni kwa Azam, lakini mpira unagonga mwamba na kurudi uwanjani. JKT 0-1 AZAM

Dk 38 Damas Makwaya wa JKT anaonyeshwa kadi ya njano baada ya kumchezea vibaya Kipre Tchetche.

Dk 34  JKT wanafika mara kadhaa langoni kwa Azam lakini Mussa Mgosi anapoteza nafasi  kadhaa za kufunga. JKT 0-1 AZAM.

Kutoka Mkwakwani Tanga - COASTAL UNION 1 - 0 JKT OLJORO


 Dk 25 Mpira haujatulia sana kila timu inacheza kwa kukamia zaidi bila ufundi.

Dk 11 Kisimba Luambano wa JKT anapiga penalti, lakini kipa Mwadini anapangua mpira. JKT 0-1 AZAM

Dk 10 Penalti...! Kipa wa Azam, Mwadini Ally anamchezea vibaya Samuel Kamuta na mwamuzi anaamuru penalti.

Dk 2 Gooo...! Khamis Mcha anaipatia Azam bao la kwanza kwa shuti hafifu akiunga krosi ya Himid Mao. JKT 0-1 AZAM

JKT RUVU V AZAM. MPIRA UMEANZA

AZAM LINE UP: Mwadini Ali, Himid Mao, Wazir Salum, David Mwantika, Jockins Atudo, Jabir Aziz, Kipre Tchetche, Ibrahim Mwaipopo, John Bocco, Humphrey Mieno, Mcha Khamis.

JKT RUVU LINE UP: Shaaban Dihile, Musa Zubeir, Kessy Mapande, Kisimba Luambano, Damas Makwaya, Jimmy Shoji, Amos Mgisa, Nashon Matal, Samwel Kamuta, Mussa Mgosi na Hussein Bunu

1 comment:

  1. Hivi ni Simba 1-0 Prisons au
    Prisons 0-1 Simba ???

    kuna muhimu kutofautisha nani alikuwa mwenyeji wa mchezo na siyo kuandika tuu ilimradi umeweka matokeo....

    ReplyDelete