Search This Blog

Thursday, February 21, 2013

KIFAA CHA UMEME KUFUNGWA KWENYE JEZI KUZUIA MATATIZO YALIYOCHUKUA UHAI WA MARC-VIVIEN FOE NA KUTISHIA MAISHA YA FABRICE MUAMBA DIMBANI

Bodi ya soka la kimataifa (IFAB) na FIFA wanajiandaa kuanza mchakato wa majaribio ya kuweka kifaa cha umeme kwenye jezi za wachezaji ili kupunguza matatizo ya kiafya kwa wachezaji yanayotokea uwanjani.
 Hatua hiyo itafanya vifaa hivyo kuwekwa kwenye pindo la shingo la jezi, ili kuweza kukusanya taarifa kuhusu mapigo ya moyo, joto la mwili na umbali ambao mchezaji anakuwa amekimbia uwanjani. Sheria za soka za sasa zinakataza mawasiliano yoyote ya kieletroniki kati ya wachezaji na makocha na watu wa wanaohusika na mambo ya afya, lakini kumekuwepo na wito kuibadili sheria hiyo ili kuleta utaratibu wa kuweka vifa vitakvyokuwa vinafuatilia maendeleo ya afya za wachezaji uwanjani, hasa kufuatiwa kutokea kwa matukio hivi karibuni ya wachezaji kama akina Fabrice Muamba, aliyendondoka uwanjani kufuatiwa kupata mshtuko wa moyo na hatimaye ikabidi aastafu soka.

Suala hili litapelekwa kwenye mkutano wa IFAB - ambayo inahusisha vyama vya soka vya England, Scotland, Wales na Northern Ireland – na FIFA katika mkutano wake wa mwaka March 3. IFAB, ambayo wanaamua sheria za mchezo, watakuwa na kura nne - moja kwa kila chama cha soka - wakati FIFA pia itakuwa itakuwa na kura nne kuamua kupitisha suala hilo. 

No comments:

Post a Comment