Search This Blog

Thursday, September 27, 2012

USAJILI WA MAMILIONI WA HULK NA WITSEL WACHAFUA HALI YA HEWA URUSI - RAISI PUTIN AINGILIA KATI

Raisi wa Russia Vladimir Putin ameingilia kati mjadala wa matumizi ya fedha katika soka la nyumbani la nchi hiyo, hasa kuihusu klabu tajiri ya nchi hiyo Zenit St Petersburg.

Mabingwa wa Russia Zenit wamekuwa kwenye mgogoro mkubwa wa ndani ya klabu katika siku za hivi karibuni, wachezaji wengi wakubwa wa timu hiyo hawana furaha baada ya klabu kutumia zaidi ya £100million katika usajili wa mshambuliaji wa kibrazil na Mbelgiji kiungo Alex Witsel muda mchache kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Zenit walimshusha nahodha Igor Denisov mpaka kwenye timu ya reserve jumapili  baada ya kukataa kucheza, akitoa masharti ya kufanyika kwa mazungumzo mapya juu ya mkataba wake. Mshambuliaji Alexander Kerzhakov pia nae alishushwa kwenye reserve timu kwa kukosa la ukosefu wa nidhamu.

Putin, ambaye ni mzaliwa wa St Petersburg alisema, Zenit wana msaada mkubwa kutoka kwa kampuni ya nishati ya Gazprom, ilikuwa inatumia fedha za kampuni kuliko za nchi.

"Mimi pia ninalalamika muda mwingine. Lakini ningependa kutoa ufafanuzi kwamba ni makampuni yanayonunua wachezaji na sio serikali," aliwaambia maofisa wa eneo hilo Jumanne iliyoipta.

""Lakini mashabiki wanataka kuwaona mastaa wa dunia, sio wale ambao ndio vyao vinaishia bali wale ambao sasa ndio muda wao."

Jumatano wiki hii, mkomunisti wa St Petersburg aliingilia kati suala hilo, akimwambia Putin kuiokoa klabu yaona kumbadili kocha wa sasa wa kiitaliano Luciano Spalleti kwa pamoja na msaidizi wake mmmojawpo kwenye benchi la ufundi anayetokea Korea.

"Tuna hali mbaya sana katika mji wa Zenit, na dhahiri timu ipo nje ya control, kumekuwepo na maugomvi  ndani ya klabu kati ya wachezaji juu ya nani anayelipwa fedha nyingi," Aliandika mkomunisti huyo kwenye barua ya wazi kwenda Putin.

Ni ngumu kutofautisha yupi sahihi au hayupo sahihi katika mtafuruku huu - wate wanakosa ubora wa adabu.

Mkomunisti huyo pia alidokezea pia kumsemea mbovu Kocha Luciano Spalletti ambaye ameizewesha klabu ya Zenit kumtwaa ubingwa wa Russia mara mbili mfululizo tangu awasili St Peterburg mwezi Disemba  2009, akimsema kuwa amezoea maisha ya kifahari sana..

"Zenit inahitaji mwalimu imara kutoka DPRK mahala ambapo michezo ni sehemu ya utafutaji wa maisha kila siku.

No comments:

Post a Comment