Search This Blog

Thursday, September 27, 2012

COASTAL WASHIKA NAFASI YA PILI LIGI KUU BAADA YA KUIFUNGA KAGERA SUGAR

Siku moja baada ya aliyekuwa kocha wao mkuu Juma Mgunda kujiuzulu, klabu ya Coastal Union ya Tanga leo imeibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Kagera Sugar katika mechi yao ya Ligi Kuu ya Bara iliyopigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.

Magoli ya Coastal katika mechi hiyo yalifungwa na Daniel Hanga na Nsa Job akaongeza mengine mawili. Mpaka refa anapuliza kipenga dakika ya 90 Wagosi walikuwa wameshinda 3-2, hivyo kupanda mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi kuu wakiwa na pointi 8, nyuma ya Simba wenye tisa baada ya kucheza mechi tatu.

Matokeo ya mechi nyingine ya Ligi Kuu ya Bara leo, Polisi Moro ilishikiliwa kwa sare ya 0-0 na Toto African ya Mwanza.

No comments:

Post a Comment