Search This Blog

Thursday, September 27, 2012

MASHABIKI NA WANACHAMA KUAMUA HATMA YA MENEJA MKUU WA SEATTLE SOUNDERS

Mashabiki wa klabu ya ligi kuu ya Marekani Seattle Sounders watapiga kura za kuamua kurefusha au kutorefusha mkataba wa meneja mkuu wa klabu yao, kitu ambacho klabu hiyo inasema itakuwa ni kura ya kwanza ya aina ya katika historia ya michezo ya Marekani.

Wanunuzi wa tiketi za msimu na wanachama wa kulipiwa, kundi la watu linalofikia watu 42,000, watakuwa na uwezo wa kupiga kura kwenye mtandao za kuamua kuendelea kumpa ajira au kumchinjia baharini  Adrian Hanauer

Hanauer alikuwa sehemu ya kundi la umiliki liloileta Sounders katika MLS mwaka 2009 huku wakitoa ahadi ya kura ya demokrasia katika kumchagua meneja mkuu.

Hii sio mara ya kwanza kwa Sounders kuwaambia mashabiki wao kupiga kura kwenye issue muhimu.

No comments:

Post a Comment