Search This Blog

Friday, August 17, 2012

HIVI NDIVYO WASHABIKI WA ARSENAL WALIVYOUMIZWA NA VAN PERSIE KWENDA MAN UNITED




 Jana nilitoa nafasi kwa mashabiki wa Arsenal kuweza kutoa maoni yao juu ya suala la uhamisho wa mshambuliaji Robin Van Persie kwenda Manchester United, mamilioni ya washabiki wa Arsenal duniani walianza kuitumia kila nafasi wanayoipata kutoa maoni juu ya uhamisho huo, wengine walimtakia kheri, wengine walimkashifu na kumpa majina ya ajabu ajabu huku wengine wakijaribu hata kuchoma hata jezi zake. Kutokana na hilo nilijaribu kutoa nafasi kwa washabiki wa Arsenal ambao ni wadau wa mtandao huu kutoa maoni yao juu ya uhamisho wa Robin Van Persie. Na haya ni baadhi ya yale niliyotumiwa.
 
 
 
 
Finley Fabregas
Habari Bw. Dauda,
 
Naandika maneno haya sio kwa kejeli au furaha, mie ni muanga mkubwa wa zoezi hili.
 
Ukija katika dawati langu la kazi nna kikombe (mug) chenye charter/log ya washika bunduki,    mwanangu wa kwanza na nnae huyo tu hadi sasa anajulikana kwa Finley Fabregas (wakati wa ubatizo wake padre wa Kanisa Katoliki pale Moro aligoma, lakini baadae akaelewa), namaanisha nini ? Hapa ni kuwa RVP katutenda km ilivyokuwa mwaka jana kwa Cesc..... ila Arsenal chini ya Mkufunzi nimwite Mchumi Mzee Arsene WENGER ni mzalishaji kwani watatokea akina van Persie wengi tu msimu huu, na pale ukiondoka kwa kajeli umeumia kwani wapi akina  Flamini, Helb nk walikuwa wakupotea leo la hasha..... akituuzi tutampiga majeruhu msimu mzima (kosa lake RVP ni kwenda siko, kwa mahasimu basi).
 
Inshalaah guners ipo na itaendelea kuwepo, acha tuumie japo mechi 3 za awali,
 
 
Na Baba Finley

Ndugu Shaffih Dauda.
  Mimi kama mshabiki wa klabu ya Arsenal ya Uingereza nimesikitishwa sana na hatua iliyofikiwa na klabu ya Arsenal ya kumuuza mshambuliaji Robin Van Persie kwenda Manchester United. Katika historia yote ya klabu ya Arsenal kuwa na wachezaji wazuri na baadae kuwauza pindi wanapotakiwa na klabu nyingine lakini hii ya kumuuza Van Persie kwenda Man United ndiyo imefunga jarada. Hii inaonyesha jinsi gani sasa ushindani na uhasimu katika mpira wa miguu umekwisha.. Kitu kikubwa sasa klabu kama Arsenal inajali mapato zaidi na sio mafanikio ya klabu.Arsenal na Man United ni maadui wakubwa katika ligi ya Uingereza mpaka ukiona viongozi wao wanakaa meza moja na kujadiliana kuuziana wachezaji ujue sasa uhasimu umeisha watu wana jali pesa. Je ulisha wahi sikia America waka kaa meza moja na Russia kujadili kuuziana silaha?Je ulisha wahi sikia ati serekali ya Afganistan ika kaa meza moja na wafuasi waTaliban kujadili kuuziana silaha? Uongozi wa Arsenal umefanya yote mabaya lakini hili la kumuuza Van Persie kwa wahasimu wao Man United halitasahauliwa na mashabiki wa Arsenal duniani kote. Kila wakati timu hizi zitakapo kutana msimu huu basi vurugu zitatokea kwa washabiki kumzomea sana Van Persie au kupigana kati ya mashabiki watimu zote mbili.Biashara ya Van Prsie toka Arsenal kwenda Man United naiona kama imekiuka misingi mingi ya uadui katika timu hizi mbili. Kwa miaka mingi mashabiki wa Arsenal watamchukia sana Van Persie kuliko wachezaji wengine waowahi kuhama kama vile Nasri,Adebayor, KoloToure, Ashely Cole, na wengineo.
DOCTOR.
MSHABIKI WA ARSENAL, STOCKHOLM-SWE

No comments:

Post a Comment