Search This Blog

Thursday, June 21, 2012

SIKU KAMA YA LEO: WAYNE ROONEY AFUNGA GOLI LAKE LA KWANZA KWENYE EURO - SPAIN WABEBA UBINGWA WAKWANZA ULAYA 1964

Baada ya kupoteza ushindi dakika za mwisho kwenye mchezo wao ufunguzi wa Euro 2004 kwa Ufaransa, England wakaanza kampeni yao vizuri kwenye mechi ya pili kwa ushindi wa 3-0 dhidi ya Switzerland.


Kijana wa miaka 18Wayne Rooney alifunga mara mbili akijitangaza kwenye ulimwengu wa soka, huku Steven Gerrard akifunga goli la tatu.


England na Rooney waliendeleza mazuri waliyoyafanya siku kama hii, walipokutana na Croatia kwenye mechi ya mwisho ya group. Lakini hayakuanza vizuri kwa vijana wa Sven Goran Eriksson baada ya Niko Kovac kufungagoli la kuongoza kwa Croatia.


Three lions walihangaika mpaka pale kwenye dakika ya 40, Paul Scholes aliposawazisha - goli la mwisho alilofunga kwa ajili ya nchi yake.


Wayne Rooney baadae kafunga bao la pili kabla ya timu mbili kwenda mapumziko. Baadae Frank Lampard akafunga bao  la nne.


Ushindi huo ulimaanisha England wameshinda mechi mbili mfululizo za Euro, ikiwa ni mara ya pili kufanya hivyo, baada ya kuwafunga Scotland na Holland mwaka 1996.


Ushindi huo pia uliweka rekodi nyingie baada ya England kuingia robo fainali kwa mara ya kwanza kwenye historia ya michuano hiyo wakati Euro inapofanyika nje ya ardhi ya England.


Pia siku kama ya leo Spain waliifunga Soviet Union na kufanikiwa kushinda kombe la Euro 1964

No comments:

Post a Comment