Search This Blog

Friday, June 8, 2012

EXCLUSIVE: MAXIMO KUTUA JUMANNE KUMALIZANA NA YANGA

Baada ya kufanya vibaya katika msimu uliopita, Yanga wameendelea kuunda timu upya, baada ya juzi kumsainisha Kelvin Yondan, leo hii timu hiyo imehamia kwenye benchi la ufundi.

Taarifa za kuaminika kutoka ndani ya zinasema klabu hiyo imemtumia tiketi ya ndege kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Marcio Maximo kwa ajili ya kuja kufanya mazungumzo ya kujiunga na klabu hiyo kwa ajili ya kuliongoza benchi la ufundi la wanajangwani kuanzia msimu ujao.

"Mpaka sasa tumefanya mazungumzo ya awali na Maximo na tumefikia makubaliano ya kimsingi, ambayo tunaweza kuja kuyakamilisha hapa nchini atakapotua siku ya jumanne wiki ijayo." - kilisema chanzo hicho cha kuaminika.

7 comments:

  1. Mhh! Kweli Manji kashindikana!

    ReplyDelete
  2. chezea manji wewe
    simba iko juta bomoa bomao karibu maximo

    ReplyDelete
  3. Yanga mko washamba kweli,, manji nani kwani? Siku zote yanga mnasajili kwa matarumbeta lakini mwisho wa siku wanaume simba tunapiga mpira. Usione rage anaropoka kuna watu wanasajili kimyakimya na habari mtaiona mwisho wa usajili

    ReplyDelete
  4. sitegemei jipya Dauda na wadau wengine wa timu mbof mbof za hap kwetu ,tupo ki emotion zaidi na siyo ki function ,tatiz la club ni saw na tatiz la timu ya taifa hata yanga wakimleta Morinyo na simba wakamchukua Phelipe Scolari hakuna kitu zaidi ya kurush rusha miguu ,kwani TP Mazembe wana kocha kutoka Brazil ?...ukiona bepari anapewa aendeshe kampuni yenye misingi ya ujamaa like simba na yanga ,jua dhahil ujamaa umetushinda na ipo siku utasikia Yanga PLC na hapo ndo tutawez kucheza mpira lakn leo hii broth ,tutaendlea kurusha rusha miguu tu....

    ReplyDelete
  5. brother shaffih nakupongeza,kwa kutupa maexlusive newzzzz ya bongo keep it up.

    ReplyDelete
  6. Maximo karibu tena tanzania japo umekuja kivingine kwani yanga kufungwa fungwa sasa basi,Hapa cannavaro pale Yondani,Hapa Meddie kagere Pale Aruna Akizimana Fadhili Niyonzima,Hapa Hamis kiiza pale Owen Kasule pia Yaw beko pale batezi utaipenda, ukizingatia yupo Maximo pale Manji Hakunaga YANGA kama hii.

    ReplyDelete
  7. Wapo wengi watakao chonga juu yako we fundisha samba tu hakuna matata.

    ReplyDelete