Search This Blog

Friday, June 8, 2012

EXCLUSIVE: NSAJIGWA YUPO KENYA ANAFANYA MAZUNGUMZO NA GOR MAHIA

Siku chache baada ya kutemwa na klabu yake ya Yanga, nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania Shedrack Nsajigwa sasa yupo nchini Kenya akifanya mazungumzo ya kujiunga na klabu kongwe ya nchi hiyo Gor Mahia.


Taarifa rasmi nilizozipata kutoka nchini Kenya zinasema kwamba Nsajigwa ametua Kenya jana na leo amekutana na viongozi wa klabu ya Gor Mahia na so far mazungumzo yanaenda vizuri na muda wowote wanaweza kufikia makubaliano na Nsajigwa akajiunga na mtanzania mwenzie ambaye walikuwa wakicheza wote Yanga na timu ya Taifa, Ivo Mapunda.

No comments:

Post a Comment