Search This Blog

Friday, June 29, 2012

BAADA YA KUSHINDWA KUPIGA PENATI - CRISTIANO RONALDO AACHWA NA NDEGE YA TIMU YA TAIFA KURUDI URENO

Cristiano Ronaldo alilzamika kukaa kwa masaa kadhaa nchini Ukraine baada ya kuikosa ndege ya Ureno kuelekea nyumbani. Nahodha huyo wa timu na mfungaji bora wa kikosi hicho, ambaye mapema juzi alikosa nafasi ya kupiga penati kwenye mchezo wa nusu fainali ya Euro 2012 dhidi ya Spain ambao walikamilisha kufunga penati zao za ushindi kabla ya Ronaldo kuifikia zamu yake - aliachwa akisikitika na kufura kwa hasira baada ya ndege kuondoka na kumuacha.

"Nilikuwa naongea na muhusika wa upangaji wa safari. Nikamwambia nataka kukaa nyuma kabisa kwenye ndege akanikubalia then nikaenda kwenye restauraunts kuchukua vyakula vyangu nilivyonunua na yeye akaiachia ndege iondoke bila mimi. Haikuwa haki."

Ingawa kocha Ureno aligundua kutokuwepo kwa Ronaldo kwenye ndege baada ya kutua Lisbon, nahodha wa ndege, Ted Mendes, hakuwa tayari kupokea lawama za kuachwa kwa Ronaldo.

"Ikiwa Ronaldo alitaka kuwemo ndani ya ndege alipaswa kuingia mapema kwenye ndege, lakin alichelewa mwenyewe."

Lakini hatimaye Cristiano Ronaldo alipata ndege ambayo ilimpeleka nyumbani kwao Ureno huku akijuta kwa kwenda kufuata misosi yake iliyomfanya achelewe ndege.

No comments:

Post a Comment