Search This Blog

Friday, May 25, 2012

SEPP BLATTER: MIKWAJU YA PENATI INAPOTEZA MAANA SOKA

Sepp Blatter - Raisi wa FIFA.
No wonder Waingereza hampendi Sepp Blatter.

Wiki moja baada ya timu ya Chelsea ya England kuifunga FC Bayern Munich kwa mikwaju ya penati na kufanikiwa kuchukua kombe la Mabingwa wa Ulaya - jana Bosi wa FIFA Sepp Blatter amesema anaona ni bora itafutwe njia mbadala wa kuamua mshindi wa mechi badala ya mikwaju hiyo ya penati.
Drogbaa akifunga penati iliyoipa Ubingwa wa Chelsea.

Blatter alisema: "Soka inakuwa inapoteza maana kabisa linapokuja suala la penati. Huu ni mchezo wa timu ya watu 11 kila upande, kwa maana hiyo linapokuja suala one against one - mchezo huo unapoteza maana yake.

"Labda Franz Becknbauer na wenzie kwenye kamati yao, wanaweza kutuonyesha suluhisho, inawezekana isiwe sasa labda baadae."

No comments:

Post a Comment