Search This Blog

Friday, May 25, 2012

SHINJI KAGAWA: KUTOKA LIGI YA DARAJA LA PILI YA JAPAN MPAKA DORTMUND - SHINJI KAGAWA SUPERSTAR ANAYEFUATIA NDANI YA MAN UNITED?S

Wakati taarifa za usajili wake kwenda Manchester United zikizidi kukaribia kuwa ukweli, ebu leo tuangalie uchambuzi wa kisoka kuhusu Shinji Kagawa.

Misimu miwil iliyopita, Shinji Kagawa alikuwa hajulikani kabisa nje ya Japan, lakini watu wale wenye macho yanayoona mbali waliona kiungo aliyebarikiwa uwezo wa kucheza soka huku akiisadia klabu yake ya Cerezo Osaka kupanda daraja la juu kwenye soka la Japan ndani ya misimu mitatu tu. Sasa yupo karibuni kujiunga na mabingwa kihistoria wa Barclays Premier league pale Theatre of Dreams - baada ya Red Devils kutuma ofa ya £13miilion kwa Dortmund.

Kagawa alikuwa ndio mjapan wa kwanza kuisaini mkataba wa level ya proffessional kabla ya kumaliza kutoka kwenye elimu ya juu ya sekondari. Akiwa na miaka 18 aliweza kupata nafasi ya kwenye kikosi cha kwanza cha Cerezo, na kujiamini kwake kukapanda sana baada ya kuwa na rekodi nzuri ya kufunga. Kagawa alifunga mabao 27 katika mechi 44 kwenye msimu wa 2009 na kuwasaidia Cerezo kurudi kwenye ligi kuu ya Japan baada ya kushuka kwa miaka 3. Lakini hakuweza kucheza sana kwenye ligi kuu ya Japan, baada ya wakala wa kijerumani Thomas Kroth kushughulikia uhamisho  ambao ulimuamisha kinda hilo kwenda Borussia Dortmnund - wakati timu hilipokuwa ikijipanga upya baada ya kumaliza ligi kwenye nafasi ya 5.

Performance yake pale Dortmund inajieleza yenyewe; kwenye msimu wa kwanza barani ulaya, Kagawa alikuwemo kikosi bora ya Bundesiliga japokuwa alitumia nusu ya msimu kuwa nje ya dimba kutokana  na majeruhi. Mwaka huu, ameweka rekodi mpya kwa Wajapan waliowahi kucheza Ulaya kwa kufunga mabao 13 kwenye mechi 32. Shinji ni hatari kila anapogusa mpira, ana uwezo wa kutengeneza nafasi kwa kutoa pasi za mwisho huku akiwa na uwezo mkubwa wa kupiga mashuti ya mbali.


Nchini kwao Japan, Kagawa ni moja ya wanasoka wenye majina makubwa sana na mara nyingi amekuwa akitumika kwenye matangazo akitangaza vinywaji pamoja video games.

Jezi yake ndio inaongozwa kwa kuuzwa, kwenye msururu wa maduka ya kuuza vifaa vya soka KAMO, huku ikitegemewa mauzo kupanda ikiwa tu atajiunga na klabu yenye umaarufu mkubwa kuliko zote duniani huko ASIA - Manchester United. Umaarufu wa Kagawa ambao kwa sasa upo sawa na wachezaji kama Yuto Nagamoto wa Inter pamoja na mshambuliaji wa CSKA Moscow Keisuke Honda.

Lakini tofauti na wenzake Nagamoto na Honda ambao wanapenda sana kutokea kwenye vyombo vya habari, Kagawa yeye ni kama Paul Scholes hapendi mambo ya kuwa karibu sana na media kwa aibu aliyonayo.

Pamoja na kuwa na miaka miwili Ujerumani, bado anaongea aidha kupitia mtafsiri wake au vyombo vya habari vya Japan ambavyo vimekuwa vikimfuata.

Ikiwa atahamia England itabidi ajipange sana ama aendelee kuufuata mfano wa Paul Scholes ili aweze kuepukana na vyombo vya habari vya nchi hiyo ambavyo vingine vimeanza kusema United wanamsajili Mjapan huyo kwa sababu za kibiashara - kuongeza mauzo ya bidhaa zao barani Asia hasa nchini Japan. Lakini  ama kwa hakika huyu ni aina ya kiungo mshambuliaji ambaye United wanamhitaji ili kuweza kukirudishia kikosi uwezo wa kutawala tena soka la England.

Ndani ya misimu miwili aliyokaa na Dortmund - amesaidia klabu hiyo kuupora utawala wa soka la Ujerumani kutoka kwa Bayern Munich kwa mara mbili mfululizo.

1 comment:

  1. Vichwa kama hivyo United tunavihitaji kweli ili kurudisha tena Title nyumbani Tranford!!

    ReplyDelete