Search This Blog

Wednesday, May 23, 2012

PHOTOS: ZIARA YANGU KWENYE MAKAO MAKUU YA BAYERN MUNICH

Leo nimefanya ziara ya kutembelea makao makuu ya klabu ya Bayern Munich hapa Ujerumani. Ni ziara ambayo ilikuwa na lengo la kuweza kupata kujifunza vitu zaidi jinsi kalbu hii inavyoendeshwa pamoja na kuweza kuona namna mazingira ya klabu hii kubwa duniani yalivyo. Kiukweli wenzetu wameendelea sana, kwa sababu wameweka umakini mkubwa katika kuziendesha klabu zao tofauti na nyumbani. Bayern Munich kupitia brand yao ya klabu yao wanatengeneza kila aina ya merchandise kuanzia mavazi mpaka vifaa vya michezo na vya majumbani kupitia logo ya klabu hiyo, na kupitia biashara hiyo hizo ndio maana haishangazi kuiona klabu hii ikiwa ndio tajiri zaidi hapa Ujerumani na pia ikiwa imetajwa kama klabu ya pili kwa thamani kubwa dunaiani baada ya Manchester United. Kwa mengi zaidi endelea kutembelea hapa,
Klabu hii pia ina mkataba wa kampuni ya magari ya AUDI - na kupitia mkataba huo wachezaji ana watumishi pamoja na watendaji wa klabu hii wote wanatumia magari ya kampuni hii. Hili hapa juu ni gari la mchezaji David Alaba ambaye hapa alikuwa akiondoka baada ya kuisha kwa mazoezi ya timu hiyo.

Hili ni gari la nahodha Philip Lahm.
Huu ndio mchuma wa Mario Gomez ukiwa umepaki nje ya jengo la makao makuu ya Bayern Munich.
Nikiwa nimesimama nje ya jengo la FC Bayern Munich pamoja baadhi ya mashabiki wa timu hiyo na walinzi wa makao makuu ya The Bavarians.
Dauda nikiutazama mchuma wa Striker Mario Gomez
Bwana Frank Ribery akiondoka kwenye gari lake.
Bidhaa zinazotengenezwa kwa nembo ya Bayern Munich na kuingizia klabu hii fedha nyingi sana. Haya ni majiko ya gesi.

Hizi ni glassi za kunywea pombe ambazo zote zimetengenezwa kwa nembo ya FC Bayern Munich.

Hapa nikiwa kwenye chumba cha kuifadhia makombe ya FC Bayern Munich.



No comments:

Post a Comment