Search This Blog

Thursday, May 10, 2012

BRAZIL YATANGAZA SHERIA MPYA KWA AJILI YA KOMBE LA DUNIA 2014 - POMBE RUKSA VIWANJANI

Seneta ya Brazil hatimaye imeptisha sheria ya kombe la dunia na kutoa guarantii kwa FIFA waliyokuwa wakihitaji juu ya kuandaa kombe la dunia mwaka 2014.

Sheria hiyo imekuja siku moja baada ya serikali ya Brazil kukutana na maofisa wa FIFA nchini Switzerland kujadili maandalizi ya nchi hiyo na kusuluhisha tofauti zao.

Sio watu wote wamefurahishwa na sheria hiyo. Vilevi vimekatazwa katika viwanja vya soka nchini Brazil tangu mwaka 2003, na baadhi ya wabunge wameonekana kuwa na wasiwasi na usalama viwanjani baada ya mabadiliko mapya yaliyofanyika katiba sheria mpya.

Sheria mpya imeruhusu uuzwaji wa pombe ndani ya viwanja wakati wa kombe la dunia na michuano ya mabara.

Uuzwaji wa vilevi viwanjani ulikatazwa baada ya matukio vurugu kuzidi viwanjani nchini humo - hivyo kuna baadhi ya wabunge wa nchi hiyo wanahisi suala hilo linaweza likahatarisha usalama.

No comments:

Post a Comment