Search This Blog

Saturday, March 3, 2012

WENGER ASHANGAZWA NA KUTUNUKIWA TUZO YA KOCHA BORA EPL


Arsene Wenger anasema kuna makosa yalifanyika wakati wa kumteua kocha bora wa mwezi huu katika ligi kuu ya England.
Boss huyo wa Gunners anapitia katika kipindi kigumu zaidi katika uongozi wa benchi la Arsenal lakini ameiongoza timu hiyo kutofungwa katika premier league katika kipindi cha mwezi uliopita wote akishinda mechi 3 na katika nne.
Arsenal walitoka nyuma na kuwafunga Spurs kwa 5-2 at Emirates Stadium wikiendi iliyopita na kujiweka katika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi huku leo wakiwa na mechi ngumu dhidi ya Liverpool.
“Ilinishangaza sana. Sikuweza kuelewa kabisa. Kama ulikuwa unasoma magazeti wiki 2 zilizopita utagundua kulikuwa na makosa katika kunipa hii tuzo. Wakati wananiambia kuhusu kuchukua tuzo hii nilidhani wanaongea na mtu mwingine nyuma yangu. Kiukweli sikutegemea kabisa kushinda tuzo hii”

No comments:

Post a Comment