Search This Blog

Saturday, March 3, 2012

RIO FERDINAND: NINGEKUWA BOSS WA FA NINGEMCHAGUA HARRY REDKNAPP KUIONGOZA ENGLAND.


Rio Ferdinand leo amefichua kwanini Harry Redknapp ni chaguo sahihi kuwa kocha wa England.
Ferdinand ambaye alitolewa kutoka timu za vijana na Redknapp wakiwa West Ham.
Aliliambia gazeti la The Sun: “Kama ningekuwa mtu ninayetoa maamuzi ningemteua Harry bila shaka.
“Unapomtumikia kama kocha wako, anakufanya ujionee kama mtu muhimu sana.”

Rio ambaye timu yake ya Manchester United inakutana kikosi cha Harry Redkanpp jumapili hii @White Hart Lane, anaamini kocha wake wa zamani na sifa na ubora wote wa kuwa kocha England.
FA inategemea kupata kocha mpya mwishoni wa premier league May 13 na wanasema kuna makocha zaidi ya mmoja wenye nafasi ya kumrithi Capello.

No comments:

Post a Comment