Search This Blog

Saturday, March 3, 2012

BALOTELLI AMKERA TENA MANCINI - APIGWA PICHA AKITOKA KLABU YA WACHEZA UCHI MASAA KADHAA KABLA YA MECHI.


Mario Balotelli anaweza kujikuta katika matatizo makubwa na kocha wake Roberto Mancini  baada ya kupigwa picha akitoka klabu ya wacheza uchi jana alfajiri.
Mancini alikuwa amepanga kumuanzisha muitaliano huyo katika mechi ya leo dhidi ya Bolton.
Na sasa kutokana na tukio la kuonekana alfajiri akitoka kufanya starehe muda mfupi kabla ya mechi ya leo anaweza kupigwa benchi .
Mancini ambaye juzi alimuonya Balotelli kuhusu tabia zake inasemekana amekarishwa na kitendo cha mchezaji huyo ambaye ndio alikuwa akimtegemea leo hii kutokana na Sergio Aguero na Edin Dzeko kuwa na uchovu baada ya kutumika katika mechi za kimataifa wiki hii.

No comments:

Post a Comment