Search This Blog

Sunday, March 4, 2012

MATCH LIVE CENTRE: SIMBA 2-1 KIYOVU: FULL TIME


19: Felix Sunzu anaipatia Simba goli la kuongoza.

24: Mafisango anakosa bao yeye na kipa.

30: Simba wanaonekana ku-relax na kiyovu wanakuja juu sasa.

32: Simba wanacheza counter attack na Emmanuel anapiga shuti kali linalopiga mwamba na kutoka nje.

35: Goaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaal, Simba wanapata bao la pili hapa, Mafisango anapiga penetration pass kwa Okwi nae anampasia Sunzu anayefunga bao la pili.

40: Kiyovu wanaonekana kutulia huku wakitafuta magoli ya kusawazisha. 

45: Mchezo ni mapumziko Simba 2-0 Kiyovu. Felix Sunzu amefunga magoli yote mawili pasi zote zikitoka kwa Emmanuel Okwi. 

45: Dakika 45 za mchezo kipindi cha pili ndio zinaanza. Kiyovu wamefanya mabadiliko ametoka Shyka ameingia Simon Okwi. 

47: Kiyovu wanapata faulo ndani 18 ya simba, lakini wanashindwa kuitumia vizuri.

50: Haruna Moshi Boban anapoteza mpira akiwa ndani ya 18 ya Kiyovu. 

55: Timu zinashambuliana kwa zamu. Huku Simba wakionekana hatari zaidi wanapoingia katika 18 ya Kiyovu. 

59; Kiyovu wanakosa bao hapa 

62: Patrick Mafisango anatoa pasi ya mwisho kwa Emmanuel okwi ambaye anawatoka mabeki wawili wa Kiyovu na kupiga shuti kali linalogonga mwamba na kutoka nje. 

65: Juma Kaseja anaokoa mchomo wa hatari hapa uliopigwa na Yusuph. 

74: Simba wanakosa bao la wazi kabisa.Patrick mafisango anapiga shuti kali na kipa anaokoa. 

75: Mwinyi Kazimoto anatoka nafasi yake inachukuliwa na Julius Mkude. 

76: Rodrigo anaingia kuchukua nafasi ya Simon Okwi aliyeumia kwa upande wa Kiyovu.

80: Juma Kaseja anaokoa hatari hapa, Kiyovu wanakuja juu sana na wakipata goli 1 lingine then Simba watakuwa wanayaaga mashindano haya.

78:  Kiyovu wanapata bao hapa

85: Haruna moshi anatoka anaingia Singano 'Messi'. 

90: Juma Kasejja anaokoa tena mchomo wa hatari hapa inakua kona 

91: Kaseja anaokoa tena mpira wa kichwa uliokuwa ukielekea golini 

92: Felix Sunzu anatoka anaingia Victor Costa, huku Juma Kaseja analala chini akionekana kuugulia maumivu.

3 comments:

  1. afe mtu,afe mmasai leo simba ushindi lazima

    ReplyDelete
  2. mbili moja au mbili bila

    ReplyDelete
  3. Hongereni sana Simba kwa ushindi nasikia pia wamecheza mpira mzuri. Maandalizi ya kutosha siku zote ndio huleta mafanikio natumai mtajiandaa vema kuwakabili waarabu mkizingatia round ijayo mnaanzia Dar na Timu za waarabu bila kuwapiga goli 3 nyumbani huwa wanakuwa na madhara sana wakiwa kwao.
    Hongereni sana.Shukrani shaffih kwa picha na maelezo.
    Mike.

    ReplyDelete