Search This Blog

Thursday, March 8, 2012

HILI ZENGWE LA UBINGWA WA LIGI YA MKOA WA DODOMA!

     
  • CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA DODOMA

    YAH:KUFUTWA KWA MCHEZO KATI YA MASKANI NA POLISI JAMII
    mada ya hapo juu yahusika kamati ya mtendaji baada yakupitia kikao cha kamati ya mashindano imefuta mchezo kati ya timu yako na timu ya polisi jamii kutokana na kupanga matokeo kwa kutumia kifungu no:19 cha kanuni za mashindano timu yako italipa faini ya sh.200000/= na viongozi wako wataitwa muda wowot
    e na kamati.

    ABUBAKAR IBRAHIM
    K/MKUU DOREFA

    HOJA YETU:tunashindwa kufahamu matokeo yetu yamefutwa kwa ushahidi upi ambao wamejiridhisha nao kwamba matokeo yamepangwa sisi tumemaliza ligi tukiwa na point 8 na magoli 7 na cda wamemaliza ligi wakiwa na point 8 namagoli 5 sisi tumecheza mechi ya mwisho tarehe 4/3/2012 lakini tarehe 6/3/2012 tumeshangazwa CDA kutangazwa bingwa leo tarehe 8/3/2012 ndio tumepewa barua yakufutwa kwa matokeo yetu zidi ya polisi jamii barua ya dorefa haioneshi ushahidi wowote wa kupangwa matokeo. wala haijatuita kutuita katika kamati yao lakini kwenye barua yao wamedai watatupa onyo tunasikitika kwa haya yanaotokea kwani dorefa inaburuzwa na kigogo wa TRA DODOMA ambayeni kiongozi wa juu wa CDA pia ni makamu m/kiti dorefa mpira umechezwa uwanjani kila mtu kaona kwanini wamlete bingwa wa makaratasi timu imetumia gharama kubwa kuwaweka vijana kambini mwezi 1 tunaomba tusaidiwe swala hili kwani lina mikono ya watu wanaoharibu mpira wa dodoma tuko radhi kudai haki yetu mpaka tone la mwisho la damu kwani kuto kudai haki yako ni dhambi

    AZIZ CHIKAULA
    KATIBU WA TIMU

No comments:

Post a Comment