Search This Blog

Saturday, February 18, 2012

ZLATAN IBRAHIMOVIC: VAN PERSIE ONDOKA ARSENAL

Robin Van Persie ameambiwa na Zlatan Ibrahimovic aondoke Arsenal kama anataka kushinda vikombe.

Nahodha wa gunners alishindwa kuisadia timu yake juzi Jumatano wakatika Gunners walipopewa kipigo cha 4-0 na AC Milan na kuweka matumaini finyu ya kuendelea na hatua ya mbele katika champions league.

Akiongea na The Sun Zlatan alisema: “Inapofikia kipindi hujashinda kombe lolote kwa miaka mingi watu wanaelewa unapoondoka kama Cesc Fabregas. Soka ni kila kitu kuhusu kushinda. Kama usiposhinda inabidi uondoke. Simjui kiundani Robinlakini nakumbuka jinsi alivyokuwa na kipaji kikubwa tangu akiwa Uholanzi – na sasa amekamilika.
“Sijui nini anafikiria kuhusu hatma yake kisoka lakini ningekuwa mimi ningejua cha kufanya tayari. Nimeshahama sana katika maisha yangu ya soka – nachukulia suala kama changamoto ya kufanya vizuri kwangu. Na nimeshashinda makombe 8 katika miak 8 na klabu tofauti katika nchi mbalimbali.
“Lakini kama utakaa sehemu moja katika maisha yako yote ni rahisi kucheza soka, unajihisi kama upo nyumbani na katika zone ambayo unakuwa comfortable kucheza soka., lakini ikiwa unahama katika sehemu tofauti inakuwa ni tofauti ni kama mtihani. Ikiwa utafanikiwa hapo ndipo unapokuwa bingwa wa kweli na hapo ndipo utakapopata heshima.”

1 comment: