Search This Blog

Saturday, February 18, 2012

SIMBA NAO WATOKA SARE NA KIYOVU KIGALI RWANDA

Wawakilishi wa Tanzania Bara katika kombe la Shirikisho (CAF Confederation Cup) Simba SC imetoa sare ya goli 1-1 na Kiyovu ya Rwanda mchezo uliochezwa nchini Rwanda.

Simba walikuwa wa mwanzo kupata goli kupitia kwa kiungo Mwinyi Kazimoto katika dakika ya 42 ya mchezo, na kupelekea Simba kwenda mapumziko wakiwa mbele kwa goli hilo moja.

Wakati mashabiki wa Kiyovu wakiwa wameshakubali matokeo ya kufungwa goli moja bila, na kuanza kutokomea uwanja katika dakika ya 90 walisazisha goli hilo na kupelekea mchezo kumalizika kwa sare ya 1-1.

Simba na Kiyovu watarejeana tena baada ya wiki mbili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam na matokeo hayo ya leo yanawapa hauweni Simba katika mchezo wa marudiano kwani watahitaji sare ya bila kufungana.

No comments:

Post a Comment