Search This Blog

Saturday, February 18, 2012

YANGA YATOKA SARE NA ZAMALEK TAIFA - AMRI ZAKI AINYIMA USHINDI




Klabu ya Dar Young African leo imeshindwa kuifunga Zamalek ya Misri kwenye mchezo wa ligi ya mabingwa wa Afrika baada ya kutoka sare ya bao moja kwa moja.
Katika mchezo huo ambao Yanga waliutawala kwa kiasi kikubwa huku Zamalek wakicheza kwa kijihami na kufanya mashambulizi ya kushtukiza, wanajangwani itabidi wajilaumu wenyewe baada ya kupoteza nafasi nyingi za magoli ya wazi.
Yanga ndio walikuwa wa kwanza kuzitingisha nyavu za Zamalek kwa goli lilofungwa na Hamis Kiiza katika kipindi cha kwanza kabla ya mshambuliaji wa zamani wa Wigan Athletic Amri Zaki aliyeingia akitokea benchi kuisawazishia Zamalek.
Kwa matokeo hayo ni dhahiri Yanga wamejiweka katika wakati mgumu atika mchezo wa marudiano dhidi ya Waarabu hao utakaopigwa wiki 2 zijazo katika venue ambayo bado haijawekwa wazi. 

2 comments:

  1. wale mababu asamoah na mwape ndio wamewauwa wenzao

    ReplyDelete
  2. wale mababu asamoah na mwape ndio wamewauwa wenzao

    ReplyDelete