Search This Blog

Saturday, February 11, 2012

WEMA SEPETU: LIVERPOOL LEO WANAKUFA 3-0: CHEZEA.... MAN UNITED

Mwanadada ambaye alikuwa Miss Tanzania 2006, Wema Abraham Sepetu amezungumzia mchezo utakaopigwa masaa machache kutoka sasa kati ya timu yake anayoipenda kwa moyo wake wote Manchester United dhidi ya Liverpool.


Wema ametabiri kuwa Liverpool watapokea kipigo cha goli 3-0  kutoka United. "Manchester United leo tunashinda kabisa, tena tunapiga wale wanaojiita majogoo wa jiji 3-0. Magoli yatafungwa na Wayne Rooney, Paul Scholes na Luis Nani."


 


"Mimi ni mshabiki wa Manchester United na nimeanza kuipenda tangu nianze kujua kama ipo ulimwenguni, nilijikuta tu naipenda timu hi. Kwa hapa nyumbani mini naipenda Yanga lakini simjui hata mchezaji mmojawapo wwa timu hiyo, lakini nikisika Yanga kafungwa labda na Simba roho inaniuma sana." aliongea Wema Sepetu.

No comments:

Post a Comment