Search This Blog

Saturday, February 11, 2012

SIMBA WAITAFUNA AZAM TAIFA LEO.


Klabu ya Simba ya Dar es Salaam leo imekata ngebe za wapinzani wao Azam FC baada ya kuwafunga katika mechi ya Vodacom Premier League, huku wana msimbazi wakitandaza soka safi katika pitch ya uwanja wa taifa jijini.

Magoli ya Simba yalifungwa na Emmanuel Okwi  katika dakika ya 31 kwa shuti hafifu lilowapita mabeki wa Azam na kumzidi ujanja kipa Mwadini Ally.

Baadae katika kipindi cha pili tena Okwi aliziona tena nyavu za Azam katika dakika ya 65, baada ya kupkea mpira mrefu uliowapita mabeki wa Azam na kumkuta Okwi aliyemchambua Mwadini na kutikisa nyavu.

Kwa matokeo hayo Simba wamerudi kileleni wakiwa na pointi 37 lakini wakiwa wamewazidi mchezo mmoja Yanga wenye pointi 34.

1 comment: