Search This Blog

Saturday, February 11, 2012

MAN UNITED VS LIVERPOOL: VITA TANO ZITAKAZOTOKEA KATIKA MECHI YA MAHASIMU HAWA


Moja ya mahasimu wakubwa wa soka nchini Uingereza Manchester United na Liverpool  zinakutana katika uwanja wa Old Trafford masaa machache yajayo.
Mechi hii itaonyeshwa live kwenye nchi karibia 200 na inatazamia kuangalia na watu wapatao millioni 900.
Kama vile haitoshi uhusiano mbaya uliopo baina ya timu hizi 2, na ukizingatia matukio yaliyotokea mechi kadhaa zilizopita, muda mchache ujao tutaona namna Luis Suarez atakavyokutana kwa mara ya kwanza na mashabiki wa United tangua alivyofungiwa mechi 8 baada ya FA kumkuta na hatia ya kumtolea maneno ya kibaguzi mlinzi wa kushoto wa United Patrice Evra.
Hivi hapa ni vita vitano vitakavyotokea masaa machache yajayo at Theatre Of Dreams.

DAVID DE GEA VS ANDY CARROLL
Golikipka kinda wa United kutoka Spain bado hajaweza kuzoea mikikiki ya English premier league.
Maamuzi na utawala wake ndani ya eneo la penati umekuwa maswali kila siku. Kosa lake la hivi karibuni ni lile wakati wa mechi ya FA @Anfield, ambapo mshambuliaji mwenye mwili mkubwa wa Liverpool Andy Carroll aliposimama mbele yake katika kona na kutengeneza pasi ya goli.
Japokuwa, uwezo wa De Gea wa kuzuia mashuti ya mbali pia umekuwa ukizua mashaka, lakini wikiendi iliyopita katika droo ya 3-3 dhidi ya Chelsea aliokoa magoli mawili ya wazi yaliyopigwa na Juan Mata na Gary Cahill na kuhakikisha United wanapata japo pointi @Stamford Bridge.
Mechi ya muda mchache ujao na kama Carroll akiwa uwanjani itatoa picha kama amejifunza kutokana na makosa aliyoyafanya katika mechi ya Anfield walipokutana na Liverpool kwa mara ya mwisho.

PEPE REINA VS WAYNE ROONEY
Hakuna golikipa aliyekuwa na clean sheet nyingi kuliko Pepe Reina mwenye 10 katika Premier league msimu huu.
Spanish goalkeeper ameendelea kuendelea kuwa nguzo ya ukuta wa Liverpool, na ana bahati mbaya kuwa kwa sasa anapambana na Iker Casillas na Victor Valdes kuwania nafasi ya kwanza katika kikosi cha Spain.
Rooney, hivi karibuni amekuwa katika form nzuri, na alikuwa ndio chachu ya mapambano ya United katika kurudisha mabao matatu katika 26 za kipindi cha pili @Stamford Bridge wiki iliyopita.
Kama ataendelea kuwa katika form aliyokuwa nayo wiki iliyopita ama kwa hakika atampa shida kubwa Pepe Reina.
ANTONIO VALENCIA VS LUIS ENRIQUE
Wakati mara nyingi Rooney amekuwa akitengeneza vichwa vya habari, iwe kwa mazuri au mabaya, Valencia siku za hivi karibuni amekuwa akitengeneza vichwa vya habari kama mchezaji bora kabisa wa United msimu huu so far.
Mecuardor  huyu amekuwa chachu ya ushindi wa United msimu huu, kwani ndiye mchezaji mwenye assists nyingi kuliko wote ndani ya United.
Kwa upande mwingine Jose Enrique anategemewa kurudi kutoka kwenye majeruhi baada ya Mhispania huyo kukuosa mchezo wa Jumatatu dhidi ya Spurs.
Enrique kwa sasa ni moja ya mabeki wa kushoto wazuri zaidi duniani, na ndio maana anatajwa kama ndio the best summer signing katika kikosi cha Dalglish, na ndio mtu sahihi wa kupambana na Tony V aliye katika kiwango cha juu.

PAUL SCHOLES VS STEVEN GERRARD
Paul Scholes amereje uwanjani baada ya kustaafu mwishoni mwa msimu uliopita, na amerudi katika wakati ambao United wamekuwa wadhaifu katika safu ya kiungo.
Anakutana na mmoja ya wachezaji wenzie wa England, Steven Gerrard. Nahodha wa Liverpool (na inawezekana ndiye nahodha ajaye wa England) ambaye nae ameipa uhai mkubwa timu yake tangu arejee kutoka kwenye majeruhi on Boxing day.
Hii itakuwa vita ya ujuzi katika kuhakikisha kila mmoja anaisadia timu yake  kushinda.
ALEX FERGUSON VS KENNY DALGLISH

Mechi ya kwanza ya Dalglish katika siti ya moto ya Liverpool iilikuwa dhidi ya mahasimu wao wakubwa Man United katika kombe la FA-raundi ya 3.
The retired manager aliitikia wito wa kumrithi Roy Hodgson akiwa anaponda raha katika boti ya kifahari, na zawadi yake kwa kukatisha starehe zake ilikuwa ni kipigo cha 1-0 walichopta @Old Trafford.

Tangu hapo, mechi zao 3 baina yao na United zote zilifanyika Anfield, huku Liverpool wakishinda 2(moja ya FA na nyingine ya Carling) na United wakipata droo ya 1-1 katika EPL mwezi October mwaka jana, mechi ambayo ndipo lilipotokea dhahama ya Suarez na Evra.
United wameshinda mechi zao 3 za mwisho dhidi ya Liverpool katika uwanja wao, na saba kati ya nane ya mwisho.
Je Dalglish atakubali kuendelea kuwa mteja wa United pale Old Trafford au Fergie ataendeleza uababe wake akiwa Theatre of Dreams?





LUIS SUAREZ VS OLD TRAFFORD
Acha tuseme tu, Suarez anakwenda kukutana na matusi yote yaliyomo katika kila kinywa cha mashabiki zaidi ya 70,000 at Old Trafford.
Haijalishi maneno yoyote watakayoambiwa mashabiki na kocha yoyote wa timu hizo mbili, au hata kama Suarez au Evra watayamaliza kwa kupeana mikono, Muruguay huyo atapata mapokezi mabaya mno tangu aanze kwenda Old Trafford.
Itakuwa ni hali ya ambayo ni vigumu kwa mwanadamu mwenye hisia kuivumilia, lakini yote itategemeana na jinsi Suarez atakavyo react katika dk 90 za mchezo.

2 comments:

  1. macho na masikio yetu yote yatakuwa ot

    ReplyDelete
  2. Nilitegemea bifu iliyopo kati ya suarez na evra ingekwisha leo lkn mambo yalikuwa tofauti ndani ya old Trafford. nini maana ya fair play katika soka? Suarez kitendo alichokifanya si cha uungwana katika soka, hali hii ndiyo iliyochangia kwa kiasi kikubwa kuwa na frustuation ktk mchezo wa leo.
    nampa ongera za dhati sana Evra kwa kuwadhihirishia mashabiki kuwa hana kinyongo. naitwa DIONIZ wa pande za SAUT-MWANZA shabiki wa ukweli wa MAN U

    ReplyDelete