Search This Blog

Wednesday, February 15, 2012

GUUS HIDDINK AZIWEKA VITANI CHELSEA NA ANZHI MAKHACHKALA




Plan ya Chelsea kumrudisha tena Guus Hiddink @Stamford Bridge inaweza ikawa imeingia mdudu baada ya matajiri wa kirusi Anzhi Makhachkala kuamua kuingia rasmi katika mbio za kuwania saini ya mdachi huyo.

Andre Villas-Boas yupo katika wakati mgumu ndani ya klabu ya Chelsea baada ya wachezaji wake kuziponda mbinu zake waziwazi katika uwanja wa mazoezi kufuatia kipigo cha 2-0 kutoka kwa Everton last weekend.

Hiddink, amekuwa ni kipenzi cha Roman Abramovich kwa siku zote, lakini mdachi huyo pamoja na Fabio Capello ni watu wanaongoza katika listi ya makocha wanaosakwa kuchukua majukumu ya benchi la ufundi la Anzhi.

Manager wa Anzhi Yuri Krasnozhan alijiuzulu wiki hii na warusi hao wanataka kocha wa hadhi ya juu kumrithi Yuri kabla ya dirisha la usajili la nchini kwao halijafungwa ijumaa wiki hii.
Hiddink aliifundisha Chelsea kwa kipindi kifupi mwaka 2009 na akamaliza na timu ikiwa top 4 huku wakishinda kombe la FA Cup.


Imefahamika kuwa sasa baada ya mfululizo wa matokeo mabovu Abramovich ameanza kukosa uvumilivu, wiki iliyopita alienda mazoezini kabla ya suluhu ya 3-3 na Man United na baadae akatumia siku 5 kati ya 6 zilizofuatia @Cobham training centre kabla hawajafungwa na Everton @Goodison Park.

Na sasa baada ya baadhi ya wachezaji kukosoa mbinu zake huku wengine wakitajwa kuwa na mawasiliano na mwalimu wao wa zamani Jose Mourinho kuhusu hali mbaya iliyopo darajani wakiwa na mchezo wa FA Cup dhidi ya Birmingham wikiendi ihayo huku wakiwa na mchezo mgumu dhidi ya Napoli.


1 comment:

  1. this blog is for man u fans it's clear like a blue sky

    ReplyDelete