Search This Blog

Wednesday, February 15, 2012

JOSE MOURINHO ATUHUMIWA NA RAISI WA PORTO KUMUHUJUMU VILLAS-BOAS



Jose Mourinho jana usiku alituhumiwa kumchimba Andre Villas-Boas kwa kutumiana meseji na wachezaji wa Chelsea.

Makocha wote wawili walipata majina wakiwa Porto chini ya uongozi wa raisi wa klabu hiyo Jorge Nuno Pinto da Costa, ambaye amesisitiza Special One amekuwa na mawasiliano ya karibu kuhusu hali ya Chelsea na wachezaji wake wa zamani.
Maneno ya Pinto da Costa yanazidi nguvu uvumi uliozuka wiki mbili zilizopita kutoka kwa mtu wa karibu wa Jose kwamba boss huyo wa Real Madrid anajiandaa kurudi Stamford Bridge.

Da Costa alisema: “Bado sijawa disappointed na namna Villas-Boas anavyo perform @Chelsea.
“Anafanya vizuri, amefuzu katika hatua ya 16 bora wa Champions league nab ado yupo katika kugombea kila ubingwa. Atapata mafanikio na The Blues kwa sababu mkataba wake sio wa muda mfupi.

“Anapaswa kuibadilisha timu kucheza katika mfumo wake autakao, lakini hawezi kufanya hivyo wakati kuna baadhi ya wachezaji bado wanatumiana na meseji na Mourinho kuhusu hali ya klabu, na mmiliki Abramovich analifahamu hili.”

Chelsea walilipa £14million kuweza kumchukua Villas-Boas kutoka Ureno akiwa Porto last summer na Pinto da Costa anasisitiza AVB inabidi aendelee na kazi ikiwa Blues watabaki katika top 4 mwishoni mwa msimu la sivyo ataenda Inter Milan.

Lakini pia Raisi huyo wa Porto anasema hakuwa sahihi kujiunga na Chelsea.
Pia wakati akiongea na gazeti moja nchini Italia, Pinto alisema: “Kitu pekee kitakachomgharimu kazi yake ni kutokufuzu kwa Champions league msimu ujao.
“Ikiwa ataondoka Chelsea, atakuwa kocha atakayefutia pale Inter Milan. Villas Boas aliondoka kwetu kutokana na ofa nzuri waliyotoa Chelsea.

“Kikubwa zaidi, ni zile fikra shida ambazo angezipata katika kuhakikisha anapata mafanikio ya Mourinho katika Champions league in 2004.
“Aliondoka kwenda Chelsea akidhani ni amepata nafasi ya upekee, ingawa kwangu niliona ni makosa kwa kuwa niljua haukuwa muda sahihi.”

3 comments:

  1. Kaka labda wengine tunavyosoma tunaelewa tofauti, je ni wapi alipomtuhumu? jamaa kasema kuwa Jose anawasiliana na wachezaji mastars....texting hakuna sehemu ambayo amemtuhumu....mimi ni Chelsea damu tunatakiwa kumpa Villa-Boas muda.

    Mday
    London

    ReplyDelete