Search This Blog

Friday, February 10, 2012

DAGLISH: FA KAMA WANATAKA KOCHA MUINGEREZA WAMCHUKUE ALEX FERGUSON



Manager wa Liverpool Kenny Dalglish ametoa ishara kwamba anadhani mpinzani wake mkubwa kocha wa mahasimu wake Manchester United, Sir Alex Ferguson, inabidi awe kocha wa England.
Baada ya kuondoka kwa Fabio Capello wiki hii, kocha wa Tottenham Harry Redknapp amekuwa akitajwa kama mtu sahihi kumrithi mtaliano Capello.

Lakini Dalglish, ambaye timu yake inaenda Old Trafford kesho, anafikiri kama chama cha soka na waingereza wanataka mzaliwa wa nchi hiyo amrithi Capello basi inabidi wamchague mwenye rekodi bora zaidi.

“Mimi hainisumbui sana hili suala la kocha ajaye wa England, ni wazi kabisa waskotishi ndio makocha wenye asili ya Uingereza wanaofanya vizuri zaidi kama makocha.”
“England wapo katika kutafuta kocha mwingine, na kama wanataka kocha mzaliwa wa Uingereza inabidi wamchukue kocha mwenye rekodi nzuri kuliko wote katika Premier League.

Dalglish aliweka wazi hakuwa anamzungumzia Harry Redknapp lakini akasema kama Redknapp atapewa jukumu hilo itakuwa vizuri.
Alipoulizwa kama alipokuwa akizungumzia kocha mwenye rekodi nzuri katika premier league alikuwa anamaanisha Sir Alex Ferguson, Dalglish alicheka na kusema “Jamani sijataja jina la mtu.”

No comments:

Post a Comment